NIJUZE NIJUZE Author
Title: TANZANIA KENYA NA UGANDA MWENYEJI AFCON 2027 RAIS SAMIA ATOA AGIZO
Author: NIJUZE
Rating 5 of 5 Des:
Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika (CAF) limetangaza rasmi nchi za Tanzania, Kenya na Uganda kuwa muandaaji wa michuano ya AFCON 202...

Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika (CAF) limetangaza rasmi nchi za Tanzania, Kenya na Uganda kuwa muandaaji wa michuano ya AFCON 2027.

Kamati hiyo Tendaji ya CAF imetangaza uoamuzi huo leo Cairo, Misri nah ii ni mara ya kwanza kwa nchi za ukanda wa Afrika Mashariki kuandaa michuano hii toka ianze.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Samia Suluhu Hassan ameagiza Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kuhakikisha inafanya maandalizi mazuri ya AFCON 2027 ikiwemo kukamilisha kwa wakati na kwa ubora, viwanja viwili vipya vya kisasa vya michezo Arusha na Dodoma

Kupitia Ukurasa wake rasmi wa Mtandao wa X, Rais ameandika:

"Tunamshukuru Mwenyezi Mungu tumefanikiwa kuwa wenyeji wa michuano mikubwa ya soka Afrika (AFCON2027), tukishirikiana na Kenya na Uganda. Nawapongeza nyote mlioshiriki kuhakikisha nchi yetu inapata fursa hii adhimu. Nawaagiza Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kuhakikisha tunafanya maandalizi mazuri, ikiwemo kukamilika kwa wakati na kwa ubora wa hali ya juu, viwanja viwili vipya vya kisasa vya michezo Arusha na Dodoma".

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top