Kampuni ya ukuzaji Mchezo wa ngumi (PAF Promotion
Entertainment Company Limited), imetangaza kuwa Bondia Hassan Mwakinyo sasa
atapanda ulingoni kuwania ubingwa wa mkanda wa Mabara wa IBA dhidi ya Julius
Munyelele Indongo kutoka Namibia badala ya Rayton Okwiri wa Kenya ambaye amepata
majeraha akiwa mazoezini.
Tayari Julius Indongo yupo Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya
pambano hilo na kesho Alhamisi Septemba 28, 2023 atakwepo kwenye viwanja vya
Leader Club ambapo mabondia wote watakaoshiriki pambano hilo watapima uzito.
Shughuli za kupima uzito zitaanza saa 3:00 asubuhi huku pambano likitarajiwa kufanyika Ijumaa Septemba 29, 2023 kuanzia majira ya saa 12:00 jioni kwenye ukumbi wa Ubungo Plaza, Dar es Salaam.
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.