Mikwaju ya penati kwa mara nyingine imeikwamisha Simba kutinga nusu fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika ikipoteza kwa penati 4-3 dhidi ya Wydad Athletic
Dakika 90 za mchezo huo wa mkondo wa pili robo fainali ulimalizika kwa matokeo ya Wydad kupata ushindi wa bao 1-0 na hivyo kuwa sare ya bao 1-1 Simba ikishinda bao 1-0 jijini Dar es salaam
Ukizungumzia Simba ya Kimataifa ndio hii tuliyoiona Morocco leo, benchi la ufundi chini ya kocha mkuu Robertinho Oliveira wamefanya kazi kubwa ya kutengeneza kikosi imara
Leo Simba imeondoshwa mashindanoni kwa kuwa ilikosa bahati tu, lakini haikuwa hivyo ndani ya uwanja. Wachezaji wa Simba leo wamemwaga jasho jingi uwanja wa Mohammed V, wanastahili pongezi
Msimu ujao bila ya shaka watarejea wakiwa imara zaidi...
SIMBA YAONDOSHWA KOMBE LA MABINGWA AFRIKA
***********************************************************
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.