NIJUZE NIJUZE Author
Title: HII SIO KUUWA VIPAJI NI KUWAKUZA KIAKILI
Author: NIJUZE
Rating 5 of 5 Des:
Na. Farhan Kihamu Jr. RAIS PEREZ wa Real Madrid aliwahi kuulizwa swali kwanini anajaza watoto wengi wadogo Real Madrid ambao uhakika wa namb...

Na. Farhan Kihamu Jr.

RAIS PEREZ wa Real Madrid aliwahi kuulizwa swali kwanini anajaza watoto wengi wadogo Real Madrid ambao uhakika wa namba ni mdogo, akawaambia Waandishi ukishaitaja Madrid maana yake ni timu kubwa yenye wachezaji wakubwa.

Rais akawauliza wachezaji wadogo wanatrain na wachezaji gani? Majibu yakawa wachezaji wakubwa, akauliza tena maisha ya Mchezaji anatumia muda mwingi mazoezini ama mechi? Majibu yakawa mazoezi ya mpira wa miguu, maana yake anafaidi vingi zaidi mazoezini.

Nikamkumbuka Brahim Diaz alivyotoka Real Madrid na kwenda Milan alikuwa hatari lakini alikuwa bench Madrid, nikamkumbuka Casemiro kutoka Real Madrid akaenda Porto, Alvaro Moratta na Marco Asensio, yes nikaelewa point ya Perez.

Nawatazama Vijana wadogo kama Denis Nkane, Abou Mshery, Nickson Kibabage, Crispin Ngushi, Kibwana na Clement Mzize ndani ya Yanga Afrika! To me hawapaswi kuwa na presha na Yanga hawapaswi kuacha kusign young talents, ni faida kubwa sana kwa Taifa! Kupitia timu kubwa Mchezaji anaandaliwa kuwa mkubwa.

Unamkumbuka Eric Johora the Keeper? Alikuwa anaozea bench tu Yanga lakini anatrain na Djigui Diarra! Ameondoka kwenda Geita baada ya misimu miwili, ameonesha kiwango bora na ameitwa National Team, Abou anakaa bench Yanga ila akiwa fit huwa anaitwa National team! Nickson sio regular lakini anaitwa National Team!

Hii sio kuuwa vipaji vya Wachezaji vijana bali kuwakuza kiakili na kimchezo, ni kuliponya taifa! Mchezaji anapotakiwa na timu kubwa acha aende, stori za kukaa bench hazimake sense.

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top