Unknown Unknown Author
Title: SIMULIZI:: NITAKUPENDA USIKU…!!!! SEHEMU YA TATU
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Chombezo: NITAKUPENDA USIKU TU Sehemu: 03 Mtunzi: Andrew Carlos Whatsap na Sms tu: 0713 133 633 Ilipoishia.. Nilijikuta kasuku wangu akinyw...
chombezo cover 1Chombezo: NITAKUPENDA USIKU TUSehemu: 03Mtunzi: Andrew CarlosWhatsap na Sms tu: 0713 133 633
Ilipoishia..
Nilijikuta kasuku wangu akinywea ghafla. Alinywea kwa uwoga wa ile hodi. Akaachia bonge la kojo juu ya mwili wa lile jimama. Akili ya lile jimama ilikuwa imeshamuhama ghafla. Lilikuwa likitoa sana macho kuangalia kitasa cha mlango.

Songa nayo sasa…
“Inamaana husikii hodi ikibishwa au” Aliongea yule jimama.

Mwili wote wa kwangu niliona kama kujawa na maji maji. Ninavyokuambia maji maji sio maji ya kunywa la hasha! ni mijasho!!. Hata mimi mwenyewe sikuweza kutambua ni mtu gani aliyekuwa akipiga hodi ile kwa fujo zote zile.
“Natoka! natoka usijali!” Niliongea kwa kujiuma.
Kwa haraka haraka lile jimama liliweza kuinuka nakuchukua khanga moko tu kama vijana wa sasa hivi wanavyoziita. Likaongoza mpaka karibia na kitasa cha mlango wake na lilipofika karibu liligeuza jicho kwangu nakunitolea macho legevu, shio!! kisha likafungua kitasa cha mlango wake.
“Unasemaje? mbona unarafu hivi hujui hapa ni sehemu ya biashara” Aliongea yule jimama.
Kwa akili na macho yangu wala sikuweza kumtambua aliyekuwa akibishana naye kwa mlangoni kutokana na kuuuzia mlango wake wote kwa utipwa wake na kichwa kukitoa kwa upande wa nje.
“Namtaka Seif ni mshkaji wangu uliondoka naye”
“Seif? Seif hapa hayupo! kwani hujui hii ni sehemu ya biashara kama zilivyo sehemu nyingine enhh”

Mabishano yaliendelea kuwa makubwa. Akili yangu ambaye mwenyekiti wake ni mwili tayari ilikuwa imeshafanya kazi nakugundua kuwa yule mtu aliyekuwa akiongea dhairi ni Jof. Kule kutetemeka kwangu nilikuweka kando kwa muda. Nikachukuwa nguo zangu nakuziridishia mwilini mwangu taratibu nakuinuka. Miguu yangu ikapata hamu ya kuinuka. Nikainuka nakusonga mpaka pale mlangoni lilipokuwepo lile jimama.
“Jof? Jof?” Nilitoa sauti.
Ni kweli alikuwa Jof tena Jof rafiki yangu ambaye ndiye alifanya juhudi nzima ya mimi kuweza kumnasa mwanamke mwenye umbile la kutisha mtaa. Umbile la kumdatisha kila kijana wa sasa nakujikuta halmashauri yake ya mwili kusisimka.

“ Dada huyu ni mwenzangu naomba niondoke naye!”
“Unasemaje wewe? Kwanza mimi dada yako? eti huyu ni mwenzangu uondoke naye, wapi?? tumemaliza?”
sikuweza kuwa na ujanja. Si mimi tu hata Jof mwenyewe hakuwa na la kuongea zaidi ya kumtolea macho yule jimama. Alikuwa na hasira sana kiasi kwamba alimfanya Jof ageuze alipotokea bila ya kuongea lolote nakutuacha wawili tena. Tuliingia ndani uku akibamiza mlango. Moyo wangu ukawa kama umewekewa pili pili tena zile pilipili mbuzi maana hata kutulia haukuwa ukitulia mara moja zaidi ya kuweweseka kwa kunisumbua.

“Haya nipe changu uende, nipee?” Aliongea yule jimama.
“Chako? kipi tena mbona sikuelewi?”
“Leo utaelewa tu kwanini ulivamia ile shoo na nilijua watu kama nyinyi wakware lazima mtakamatika tu hamkosi nyie”
“Kama ni hela mimi sina labda mpaka nyumbani”

Sina shida na pesa yako nimekwambia nipe changu namaanisha nipe mashine yangu maana umenikoboa wewe bado kunisaga tu”

Sikuwa na hamu tena ya kuendelea kumchokoza kasuku wangu aweze kudonoa. Alikuwa ameshajipumzikia. Alikuwa ameziba masikio yote hata zile kelele za jof akigonga mlango hakuzisikia. Achana na hiyo hata kelele za jimama likidai tuendelee hakuweza kusikia kabisa. Kwa ninavyomjua angali sikia ni lazima angelitoka japo kwa kutuna kama afanyavyo siku zote awapo na ugumu.
“Hapana siwezi embu ona” Nililalamika.
Nilimvulia suruali yangu ili aweze kushuhudia yaliomo. Hakutaka kabisa kuamini kama kweli kasuku wangu amepitiwa na usingizi fofofo. Akajitahidi sana kumuamsha kwa kumshika na kumtikisa tikisa lakini wapi. Bati!! Haikusaidia lolote si kwa kuamka tu bali hata kwa kutoa miguu yake miwili. Miguu yake ilikuwa ndio kwanza imesinyaa mithili ya kifaranga cha kuku kikinyeshewa na mvua. Mawazo mgando yakanijaa. Ninapokwambia mawazo mgando sio yale ya mtindi? hapana!! Namaanisha mawazo ya kulichukuwa kwenda kumpelekea na Jof naye alifaidi kama nilivyolifaidi mimi. Kuna wakati mawazo mgando yalinielemea kichwani ikafikia hata hatua ya kuwaza kulisafirisha hata kesho nikaishi nalo kwetu Iringa kwenye mashamba ya vitunguu na nyanya!
“Sijui litakubali? Hapana litazingua tu!” Nilijiuliza kimoyomoyo na kujijibu mwenyewe.
Nilikuwa kama mtu aliyesafirishwa na mawazo tena nchi ya mbali bila kuwa na tiketi a ndege wala basi. Akili nikairudisha toka safari ya muda niliokuwa nimesafiri nakuliangalia tena jimama langu ambalo macho yake legevu bado yalikuwa yakiomba njia kutazamana na macho yangu angavu.
“Kwanini unanifanyia hivyo” Lile jimama safari hii lilibadilisha kabisa sauti. Sauti ile ya kuweza kumtoa nyoka pangoni. Kwa mara ya kwanza aliniongelesha kwa sauti ya kimahaba na jicho akililegeza.
“Nimekwambia nahitaji unisage kwanini haisimami hii mashine yako”
“Ukiona hivyo ujue imechoka”
“Eti niiini”
“Kama ulivyosikia!! ndio imechoka!”

Ilinibidi kumwambia ukweli lakini ndio kwanza kwa jimama ni kama kumpigia mbuzi gitaa na matarumbeta aweze kuucheza muziki. Kale kahali ka kunibembeleza ambacho alikaonesha kwa sekunde chache akakachukua nakukaweka pembeni. Ule mwili wake ulivyo tipwa tipwa akasimama nao mpaka juu. manyama nyama ya pembeni mwa tumbo lake yakasalimiana na manyama nyama ya tumboni mwake. Yakapiga makofi kwa pamoja yakitikisika. Akaniinamia tena mpaka chini nilipokuwepo kwa mara ya pili. Tukatazamana!! Akanong’ona!!
“Sipendi nikuache hivi hivi nitakusindikiza mpaka kwako nikapajue, sijawahi kukutana na mashine kama hizi maishani mwangu. Wewe ni zaidi ya mashine kwangu na roho itaniuma sana endapo nitaikosa mashine hii japo kwa siku mbili zinipite”

Yule jimama alikuwa tayari ameshadata kupitiliza. Kudata kwa siku moja tena akiwa kama Malaya anayejiuza. Nilijiuliza maswali mengi sana pasipo kupata jibu hata kama ungelikuwa wewe maswali kama haya ni lazima yangekuchanganya kichwa. Sikutaka wala kuweza kuamini kuwa toka ameianza hii kazi yake ya ukahaba eti leo ndio kakutana na mashine yenyewe. Jibu kwangu likawa hapana!
Kasuku wangu alimnyima sana raha hata na mimi sikutaka tena kuweka hisia aamke. Nilijua tu endapo akiamka angekutana na dhahama kali. Idadi ambayo amekwishatapika kwa usiku mmoja tu ilikuwa ni idadi kubwa sana kwake.

Alinipa ruhusa ya kuweza kuiweka suruali yangu vizuri nayeye pia akaufunika ule mwili wake kwa nguo zake kisha akafungua mlango na kutoka naye.
“Umesema unakaa mtaa upi?”
“Mtaa wa tatu kutoka hapa”
“Hapa mpaka nihakikishe nimekujua kwako maana vijana wa siku hizi nyie mhh, haya niambie mapema kama kuna ka demu kako mapemaaa atambue huko”
“Hapana sina demu wala mke”
“Utakuwa unajidanganya mwenyewe kwa maana hata mama mwenye nyumba wako leo atajua kuwa umenioa wewe ngoja tufike tu!”

Miguu yangu iliokuwa imepambwa kwa kandambili chafu za uswahilini iliweza kukatiza chochoro ambazo kiukweli hata sikuweza kuzijua vizuri japokuwa na umeme kwa safari hii ulikuwepo. Visichana vidogo dogo vilikuwa vimetanda eneo lote. Havikuwa vikicheza bali vilikuwa kazini vikijiuza miili yao. Vimacho vyao viliwalegea sana mithili ya mtu aliyekula kungumanga!! Vilikuwa vikinuna sana kwa kuniona nikiwa na lile jimama. Vikatoa cheko la haja kwa pamoja!!
“Enheee heee heee haya wale wa wahaya! spare tyre hizoo zimeshakwisha kazi yake zinachukuana zenyewe kwa zenyewe”
Waliendelea kunong’ona wenyewe kwa wenyewe wakitishangaa tukikatiza mitaa. Yule jimama hasira zikampanda pasipo mimi kujua. Kelele za vile visichana na kebehi zao zikamkuna. Akajiona kama yupo uchi. Akanivuta mkono wangu kuonesha ishara kuwa nisimame. Nikatuliza kandambili zangu. Wima!!
Mnasemaje nyie vitoto vya juzi” Akavisema vile visichana.
“Unajua vitoto wewe? vitoto vipo kwao vimejilalia na vingine vinanyonya hapa kazi tu nenda mkachome mahindi na mkulima mwenzako huyo”

Maneno yalizidi kumuingia yule jimama. Hata na mimi yalinikuna kutokana na uchafu niliokuwa nao japokuwa uchafu wangu ulifunikwa kwa kutembea na jimama njiani.
“Nitawateketeza nyie vitoto” Aliongea yule jimama.
“Mteketeze huyo uliokuwa naye tena kwa ukimwi maana sijui hata kama mzima wewe?”

Maneno yale yakawa yameshayachosha masikio ya jimama. Likashindwa kuvumilia zaidi ya kufura hasira. Likachojoa vito vyake vya thamani.
“Seif wacha nikawaoneshe adabu”
Likanikabidhi micheni yake ya shingoni na mabangili ya mikononi. Likavua viatu vyake vya kuchomeka kisha likavisogelea vile vitoto.
Havikuwa vikiogopa kwani ndio kwanza vilikuwa katika kunogewa katika kupuliza moshi wa sigara sambamba na kulitukana lile jimama langu.
**********

:: Unavyodhani ni nini kitaendelea hapo? Je Jimama litatoka salama hapo kwa hivyo vitoto vikahaba?
:: Vipi Seif atasubuiri au ndio atakimbia na vitu alivyokuwa navyo mpaka geto kwake. Na kuhusu hilo Jimama vipi kweli safari ya kwenda getto kwa seif itatimia?
:: LIKE nyingi na COMMENT bila kusahau SHARE ndizo zinafanya Chombezo hili kuwa likitoka kila siku na kwa muda muafaka. Hakika si ya kukosa hii.
::: ANGALIZO :::
Chombezo hili litakuwa likitoka kila siku kuanzia saa MOJA KAMILI ASUBUHI.

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top