NIJUZE NIJUZE Author
Title: ONYANGO ANYAKUA TUZO YA LUIS MIQUISSONE
Author: NIJUZE
Rating 5 of 5 Des:
B EKI kisiki wa Simba raia wa Kenya, Joash Onyango, amekabidhiwa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwezi Machi wa kikosi hicho baada ya kupigiwa kura...

BEKI kisiki wa Simba raia wa Kenya, Joash Onyango, amekabidhiwa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwezi Machi wa kikosi hicho baada ya kupigiwa kura nyingi na mashabiki.

Onyango amewashinda Aishi Manula na Luis Miquissone kwenye kinyang’anyiro hicho cha kuwania tuzo hiyo inayodhaminiwa na Kampuni ya Emirates Aluminium Profi le.

Beki huyo anakuwa mchezaji wa pili kutwaa tuzo hiyo iliyoanza kutolewa Februari, mwaka huu na kubebwa na Luis. Mbali na kupewa tuzo, Onyango amekabidhiwa kitita cha shilingi milioni moja.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo Onyango alisema “Tuzo hii itaongeza morali kwangu na kwa wenzangu katika hali ya kuendelea kupambana kwa ajili ya miezi mingine ijayo.

Kwa upande wa Ofisa Mahusiano wa Emirates, Issa Maeda, amesema "Tutaendelea kutoa tuzo hizi hadi mwisho wa msimu, mambo yakiendelea kuwa mazuri, msimu ujao tunaweza kuwepo tena na kuongeza dau kufikia shilingi milioni tano".


 

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top