RAIA WA JAPAN AKUTWA KAJINYONGA NDANI YA CHUMBA CHA UCHUNGUNZI

Raia wa Japan
Katika hali isiyokuwa ya kawaida mtu mmoja Raia wa Japan aliyekuwa mfanyakazi wa kampuni ya Konoike inayoshughulika na mradi wa maji vijijini, amekutwa amejinyonga katika chumba cha kufanyia uchunguzi wa udongo, bila kuacha ujumbe wowote, jambo ambalo limeibua mshangao kwa wananchi wa Tabora na wafanyakazi wenzake. 

Akidhibitisha tukio hilo, Kamanda wa Polisi mkoani Tabora Kamishina Msaidizi Hamis Suleiman, amemtaja marehemu kwa jina la Akihila Takahashi(49), akidai kuwa tukio hilo ni la kushangaza, na ni la kwanza mkoani Tabora mtaalamu na Raia wa Kigeni kujinyonga, huku akisema kuwa uchunguzi wa kina unafanyika.
Raia wa Japan
Wakiongea na Lindiyetu.com kwa masikitiko eneo la tukio ambapo Mjapan huyo alijinyonga kwa kutumia kamba, baadhi ya wafanyakazi wenzake walioshuhudia mwili wa marehemu ukiwa umening’inia wamesema kuwa, jana yake walikuwa naye kazini kama kawaida.
Previous Post Next Post