Unknown Unknown Author
Title: SOMA MAKALA YA MAHOJIANO YA MWANDISHI WETU NA ABDULAZIZ AHMEID MGOMBEA UBUNGE MTARAJIWA JIMBO LA LINDI
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Abdulaziz Ahmeid Mwandishi wa habari wa kituo cha Televisheni cha Channel Ten Akifanya mahojiano na mwandishi wetu Nyumbani kwake. N...
Abdulaziz Ahmeid
Abdulaziz Ahmeid Mwandishi wa habari wa kituo cha Televisheni cha Channel Ten Akifanya mahojiano na mwandishi wetu Nyumbani kwake.

Na AHMAD MMOW-LINDI
Hivi karibuni mwandishi wa habari wa kituo cha televishen cha channel ten, Abdulaziz Ahmeid akiwa mjini Lindi Mbele ya waandishi wa Habari wenzake wa vyombo mbalimbali vya habari alitangaza nia ya kuomba ridhaa ya Chama Cha Mapinduzi ili ateuliwe kugombea ubunge katika jimbo la Lindi mjini, ambalo kwa sasa mbunge wake ni Salum Barwany wa CUF-Chama Cha Wananchi.

Mtandao huu ulifanya mahojiano na Abdulaziz, Mtoto wa aliyekuwa mwanasiasa na mtendaji wa Chama Cha Mapinduzi katika mikoa mbalimbali, Marehemu Ahmed Abdulaziz.

Yaliyojiri kwenye mahojiano hayo yaliyofanywa na mwandishi wetu Ahmad Mmow, fuatilia na soma makala haya:-

Mwandishi: Abdulaziz Wasomaji na mimi mwenyewe napenda kujua historia yako japo kwa ufupi.

Abdulaziz: Mimi ni kijana mwenye haki ya kuitwa kijana, maana nina miaka 41 tu,nilizaliwa mwaka 1974, Nina Mke na Watoto watatu.
Elimu yangu ni ya kidato cha nne ambayo niliipata katika shule ya sekondari ya Mkonge iliyopo hapa Lindi Kuanzia mwaka 1990 hadi 1993.
Elimu ya msingi nilisoma katika shule tofauti Maana Marehemu baba Yangu alikuwa mtumishi wa Chama Cha Mapinduzi, alikuwa mhasibu wa CCM  mkoa. Kwa hiyo alipokuwa anahamishwa kutoka kituo kimoja na kuhamia kituo kingine tulikuwa tunahama wote.

Mwandishi: kwahiyo elimu ya msingi ulipata katika shule gani?
Abdulaziz: Kabla ya shule ya msingi nilianza na elimu ya awali, chekechea katika shule ya Parish inayomilikiwa na kanisa katoliki pale Mtwara.

Baba kwa muda huo alikuwa mhasibu wa CCM mkoa wa Mtwara.
Ilikuwa 1979 hadi 1980. Nakumbuka Mwaka 1981 nirudia tena kusoma elimu ya awali katika skuli ya Kidutani, Zanzibar baada ya marehemu baba  kuhamishiwa mkoa wa mjini magharibi kama Mhasibu wa CCM Mkoa.

Mwaka 1982 nilianza darasa la kwanza katika skuli ya Kisiwandui hukohuko Zanzibar(1981-1985).

Mwaka 1985 Kwa Mapenzi ya Mungu Baba alifariki ghafla  akiwa ofisini Kwake, ofisi ya CCM Kisiwandui Baada ya kifo hicho Tulilazimika kurudi kijijini kwetu Mchinga Wilaya na Mkoa wa Lindi
Hivyo  Baada ya kifo cha  Marehemu baba ambaye alizikwa katika kijiji hicho, Mimi, dada yangu Salma Ambae nae alifariki 1995 pamoja ndugu yangu ALLY Tulibaki kijijini.

Yaani Mwandishi Hapa nalazimika sana kukishukuru sana Chama Cha Mapinduzi Makao Makuu kwa kukodi Ndege Aina ya Forker ya shirika la ATC kuleta maiti ya baba Kutoka Unguja hadi kiwanja cha Ndege Cha Kikwetu na Ndege hiyo ililala kiwanjani hapo hadi siku ya Pili kuwasubiri waombolezaji waliotoka Unguja kuja Kuzika ili kuwarudisha hakika ulikuwa Mchango mkubwa kwa waliokuwa karibu na marehemu pamoja na waliokuwa wakifanya nae kazi pamoja.

Pia Jitihada zilizofanywa na Bi Fatma Mikidadi ambaye alikuwa ni mke wa baba yangu mkubwa Marehemu Basheikh Mikidadi (MNEC) Kabla ya kifo chake 1984 Bi Fatma Mikidadi alifika kijijini akiwa Mratibu wa elimu Lindi aliwasiliana na Marehemu Mama Yangu  na akatuchukua mimi na dada yangu ili tukaendelee na masomo katika shule ya msingi ya stadium iliyopo katika mji wa Lindi.

Namshukuru sana alipotoa wazo la kurudia darasa toka la nne na kuanza Darasa la Tatu Aug 1985 ambapo Nilisoma na kumaliza elimu ya msingi katika shule hiyo mwaka 1989.

Mwandishi; Umetangaza nia ya kuomba ridhaa ya chama chako ili uteuliwe kugombea ubunge. Lakini jimbo hili lina mbunge, na kwa mujibu wa CCM muda wa wanachama wake kutangaza nia haujafika.

Je wewe umeamua kupuuza marufuku hiyo ya CCM unayotaka kuomba ridhaa yake?

Abdulaaziz: Mwandishi hili ni Jimbo huru Bwana:Nikweli CCM kimepiga marufuku kutangaza nia kabla ya muda kufika, lakini siyo kwa majimbo yote.Bali kwa majimbo yale ambayo wabunge wake wanapitia CCM tu Hivyo Jimbo la Lindi mbunge wake hatokani na CCM, ruksa kutangaza Nia na kuanza Mambo ili mradi usivunje kanuni na kuchochea Migawanyiko. Lakini wapo wanachama wametangaza nia ya kugombea urais wakati rais aliye madarakani hajamaliza muda wake hii inatokana na Rais huyo kutogombea Tena kipindi kijacho.

Kwa hiyo sijakiuka taratibu, kanuni wala sheria za CCM.

MwandishiNini kimekusukuma kugombea ubunge, tena katika jimbo la Lindi mjini badala ya jimbo la Mchinga ambalo kwa mujibu wa maelezo yako, ndiyo nyumbani kwenu?

Abdulaaziz: Kwanini nataka kugombea Lindi mjini badala ya Mchinga Mwandishi Hapa Lindi mjini ni nyumbani pia,uliza wana Lindi watathibitisha Na hata wazazi wangu Mchinga ni kwao ila makazi na maisha yao ni Mjini Lindi labda Kuhusu kilichonisukuma kutaka kugombea ni Kuwepo kwa maendeleo duni na hafifu ya jimbo la Lindi mjini.

Hayo ni matokeo ya Kukosa Uwakilishi ikiwamo mbunge ambae Mwaka 2010 wananchi wakiwemo wana CCM Kujenga Imani nae kwa kubadilika na kutoa ridhaa kwa CUF

Mimi niliomba ridhaa ya chama changu kugombea, lakini kura hazikutosha kwenye kura za maoni. Hata hivyo kero za wananchi hazijapata uvumbuzi hadi sasa.
‘Nilipotafakari nakujipima nikagundua naweza kuzishugulikia changamoto na matatizo yaliyopo.

Mwandishi: Umesema jimbo la Lindi linachangamoto nyingi, Unaweza kuzitaja japo kwa uchache?

Abdulaziz: Changamoto ni nyingi ikiwamo kuporomoka kwa kiwango cha elimu katika jimbo la Lindi na mkoa mzima wa Lindi kwa jumla.
Mkoa huu uliwahi kushika nafasi ya kwanza kwa ufaulu wa watoto wa darasa la saba. Lakini tumeporomoka na kuwa mkiani. Tatizo ni uongozi uliopo kutokuwa na mikakati sahihi ya kulipatia ufumbuzi tatizo hili kwa kuanza kutafuta sababu.

Viongozi waliopo ikiwamo mbunge hawaoneshi kusikitishwa wala kujali hali hii. Hivi jiulize kama wangekuwa serious kulitafutia uvumbuzi isingewezekana baadhi ya shule za hapa Lindi mjini hazina vyoo vya kutosha, hali inayosababisha waalimu na wanafunzi kushirikiana choo hii imejionyesha katika shule ya sekondari ya Angaza....

Migogoro isiyokwisha na ya mara kwa mara  ndani ya baraza la madiwani la halmashauri ya manispaa ya Lindi.

Badala yake mbunge ambaye ni sehemu ya madiwani anakuwa nichanzo cha migogoro.

Mwandishi: Kama chama chako kikikupa ridhaa na hatimae kuwa mbunge. Je utayawekea kipambele mambo gani?

Abdulaziz: Kimsingi jimbo la Lindi linachangamoto nyingi, lakini mimi nitaanza kwanza  kwa kusimamia nidhamu ya matumizi ya fedha katika manispaa. pili kuunganisha makundi yanayo hasimiana na kusababisha migogoro isiyo na tija kwa wananchi. Baada ya hapo nitaanza na miundo mbinu ya barabara, maji, afya na elimu, jambo ambalo litakuwa miongoni mwa mambo ya awali kuyashugulikia.

Kwani elimu ndiyo msingi wa maisha. Kwajumla changamoto ni nyingi, lakini ili kufanikiwa kuzishugulikia ni ushirikiano nitakaopewa na wana Lindi. Ukiwa kiongozi nilazima uwe kiongozi wa watu, ambao nao wanajibu wakukupa ushirikiano.

Mwandishi: Ungozi mzuri unategemea uzoefu. Wewe unazoefu wowote? 
Abdulaziz: Kuwa mwandishi wa habari ni uzoefu pia kwani ninachanganyika na makundi mbalimbali na watu wenye rika nyadhifa na kazi mbalimbali nasijawahi kulalamikiwa katika utendaji na utekelezaji wa majukumu yangu ya uandishi wa habari.

Pia nilipokuwa sekondari nilikuwa katibu wa umoja wa vijana wa ccm tawi la sekondari ya Mkonge. Utaona kuwa nimeanza kuwa kiongozi nikiwa umri mdogo. Kama hiyo haitoshi tangu nijiunge na kuwa mwanachama wa klabu ya waandishi wa habari nimekuwa kiongozi nikianza na ukatibu msaidizi mwaka 2008, wanachama walionesha imani na kunichagua kuwa mwenyekiti wao, kulikotokana na umahiri wangu hususani katika UMOJA  kwa Vilabu vya waandishi wa habari nchini.

Mwandishi: Kwahiyo unawahaidi nini wananchi wa jimbo la Lindi iwapo watakuchagua nakua mbunge wao?
Abdulaziz:Watarajie maendeleo ya kasi yatakayotokama na rasilimali zilizopo Lindi na mji wa lindi unakua kwa kasi na kuna kilasababu nyingi lakini kubwa zaidi raslimali ya gesi asili iliyogunduliwa katika kanda hii. Gesi imepandisha thamani ya ardhi na maliasili nyingine.

Kwahiyo kinachohitajika nikiongozi makini tu, lazima Lindi itasonga mbele na kuondokana na udumavu uliopo sasa. Inasikitisha kuona raslimali zilizopo zinazalisha migogoro badala ya maendeleo. Utakumbuka kuna mgogoro wa ardhi umesumbua sana hapa Lindi. Hali hiyo imetokana na kukosekana uongozi makini.

Mwandishi: Mara nyingi watu wanapoomba uongozi wamekuwa natabia ya kuhaidi mambo mengi mazuri, lakini wakichaguliwa wanageuka. Hilo lipoje kwako iwapo utachaguliwa?
Abdulaziz: Hilo lipo na bado ndilo lililowafanya wana CCM  na wananchi wa Lindi, mwaka 2010 wamchague mgombea wa upinzani ambaye alihaidi mambo mengi mazuri, wananchi wa Lindi walijazwa matumaini. Lakini baada ya kuchaguliwa amewageuka anatenda kinyume na alivyokuwa amehaidi.

Kwangu haitakuwa hivyo, ndiyo sababu nimesema mafanikio ya kiongozi yanatokana na ushirikiano uliopo na wananchi ikiwemo namna yeye mwenyewe atakavyowashirikisha pamoja na  kupokea ushauri.
‘Hayo yatafanyika ukiwa karibu na wananchi naomba Wasiwe na shaka, mimi nitabaki kuwa mtu wa Lindi nanitaendelea kuishi Lindi.

Mwandishi: Naamini wana CCM wenzako na wananchi wa Lindi, wamekusikia. Nakutakia mafanikio katika harakati zako za kutaka kuwawakilisha wananchi wa jimbo la Lindi mjini.

Abdulaziz: Ahsante, nashukuru.

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top