SIMBA SC YABANWA MBAVU KWA MKAPA

Jean Charles  Ahoua (simba sc) akijaribu kumtoka Akaminko (Azam) katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa katika dimba la Benjamin Mkapa Februari 24 2025.
 Gibril Sillah (Azam Fc) akijaribu kumtoka Mohammed Hussein 'Zimbwe Jr' (Simba Sc) katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa katika dimba la Benjamin Mkapa Februari 24 2025.
 Elie Mpanzu (Simba Sc) akijaribu kuwapiga chenga mabeki wa Azam Fc katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa katika dimba la Benjamin Mkapa Februari 24 2025.
Feisal Salum (Azam Fc) akijaribu kuwapiga chenga mabeki wa Simba Sc katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa katika dimba la Benjamin Mkapa Februari 24 2025.

Na. Mwandishi Wetu Dar es Salaam

Mchezo wa Ligi Kuu kati ya Simba na Azam FC uliofanyika uwanja wa Benjamin Mkapa umemalizika kwa sare ya 2-2.

Huu ulikuwa ni Mzizima Derby, mechi yenye ushindani mkubwa kutoka kwa kila timu. Simba walitawala mchezo kwa ujumla, huku Azam FC wakitekeleza mashambulizi ya kushitukiza.

Azam FC walikuwa wa kwanza kupata bao la uongozi dakika ya kwanza kupitia kwa Gibril Sillah, aliyemalizia shambulizi la kushitukiza.

Simba walijibu mapema dakika ya 25 kupitia kwa Elie Mpanzu, ambaye alifunga baada ya kazi nzuri iliyofanywa na Kibu Denis.

Kipindi cha pili kilikuwa cha upinzani mkali, ambapo Simba walifanikiwa kupata bao la pili dakika ya 76. Abdulrazak Hamza alifunga kwa kichwa baada ya mpira wa adhabu uliochapwa na Jean Charles Ahoua.

Hata hivyo, Azam FC walifanikiwa kusawazisha bao hilo dakika mbili kabla ya kumalizika kwa mchezo. Zidane Sereli alifunga kwa pasi nzuri kutoka kwa Feisal Salum, baada ya kumzidi mbio nahodha wa Simba, Mohammed Hussein 'Zimbwe Jr'.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post