Jengo jipya la Ofisi za Uhamiaji Mkoa wa Lindi limefunguliwa leo hii April 26, 2023 na Mkuu wa Mkoa wa Lindi Bi Zainab Telack |
Mkuu wa Mkoa wa Lindi Bi Zainab Telack amezindua jengo la Ofisi za Uhamiaji Mkoa wa Lindi leo hii katika sherehe za maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 59 Muungano wa Tanzania.
Bi Zainab ameipongeza Wizara ya mambo ya ndani kwa kuweza kujenga jengo hilo ambalo litarahisisha huduma katika mkoa huu kwa wananchi.
Akizungumza katika maadhimisho hayo Bi Zainab amesema
“Imekuwa bahati kubwa leo hii kuzindua jengo hili kwani Linaenda kupendezesha mji wetu lakini pili linakwenda kufanya urahisi wa utendaji kazi wa jeshi letu la Uhamiaji”
Jengo Hilo limegharimu kiasi cha Tsh 2,228,396,218.46
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.