Achana na taarifa zilizozagaa kwenye mitandao ya kijamii zilizodai kuwa Rivers United wanakabiliwa na ukata na hivyo wanaweza kuwasili nchini Jumamosi na kuondoka siku ya Jumatatu baada ya mchezo dhidi ya Yanga ambao utapigwa uwanja wa Benjamin Mkapa siku ya Jumapili
Wachezaji wa River United wakiwa Airpot Nigeria tayari kwa kuanza safari ya Kuja Dar es Salaam kuwakabili Young Africans
Hizo ni mbinu tu wanajaribu kutumia ili ionekane kama wamekata tamaa na mchezo wa marudiano
Habazi za uhakika ni kuwa Rivers United tayari wameondoka huko Nigeria na watawasili nchini wakati wowote kwa ajili ya mchezo dhidi ya Yanga
Wananchi hawapaswi kuingia kwenye mtego wa kuaminishwa kuwa Rivers United wamekubali kipigo na hivyo wanakuja kukamilisha ratiba tu
Jambo la uhakika ni kuwa mchezo wa Jumapili utakuwa mgumu, Yanga itapaswa kuchukulia kama ni mechi mpya pasipo kujali matokeo ya mechi ya mkondo wa kwanza
Habari njema ni kuwa baada ya ushindi wa Nigeria wachezaji na benchi la ufundi walitarajia hicho walichokifanya Rivers United. Wamefeli kwani watarajie kukutana na Yanga yenye njaa ya kutinga nusu fainali
Baada ya ushindi wa Nigeria, kocha Mkuu wa Yanga Nasreddine Nabi alibainisha kuwa bado hawajafuzu nusu fainali na kuwa ili kufanikisha hilo wanapaswa kushinda dhidi ya Rivers United baada ya mechi zote mbili
Mechi iliyopigwa Nigeria ni kama dakika 45 za kwanza na hii itakayopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa Jumapili ni dakika 45 za pili
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.