DIAMOND PLATNUMZ AWAOMBA RADHI MASHABIKI WA WASHINGTON DC BAADA YA SHOW YAKE KUSHINDWA KUMALIZIKA

Mkali wa Bongo Fleva, Mshiriki wa tunzo za BET katika kipengele cha  Msanii Bora wa Kimataifa toka Africa na Hit Maker wa wimbo wa "Make me Sing" Diamond Platnumz ameweza kuonesha kuumizwa kwa kushindwa kumaliza kuperfom katika show yake iliyofanyika Nchini Marekani.
Diamond Platnumz
Mkali huyo wa Bongo Fleva amesema imemsikitisha sana lakini ilikuwa hakuna namna kwani ni sababu zilizokuwa nje ya uwezo wake.

Kikubwa kulicho msikitisha ni kwamba hakuweza kupafomu nyimbo zake kali kama "Nasema nawe", "Nana", "Number One Remx", "Mdogo mdogo", "Make me Sing", "Bado", "Kigoma" na "Zigo Remix"

Amesema alipanga kutumbuiza nyimbo 27 lakini aliweza kuimba nyimbo 19 tu na wimbo wa Mwisho ulikuwa ni "Utanipenda"

Mtazame hapa akifunguka:

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post