TAZAMA HAPA HASIRA ZA MASHABIKI WA CRISTIANO RONALDO WALICHOFANYA BAADA YA KUSHINDWA BALLON d'Or

Lionel Messi na Cristiano Ronaldo
Usiku wa January 11 Staa wa Barcelona Lionel Messi aliandika historia nyingine baada ya kushinda tuzo ya Ballon d’Or kwa mara ya tano akiwashinda wapinzani wake Cristiano Ronaldo pamoja na Neymar.

Mashabiki wa Cristiano Ronaldo katika mji wa Madeira alipozaliwa staa huyo hawakufurahishwa na ushindi wa Messi..walichofanya waliamua kwenda kwenye sanamu lake lililopo katikati ya mji na kuanza kulichafua kwa kuandika jina la Messi.

Cristiano Ronaldo
Sanamu la Cristiano Ronaldo likionyeshwa kwa nyuma lilivyochafulia huku likiandikwa jina la Messi
Mashabiki hao walichafua sanamu hilo lililowekwa mwaka 2014 kwa kutumia rangi nyekundu wakiandika jina lake pamoja na namba 10 ambayo imekuwa ikitumiwa na Messi kama ishara ya kuchukizwa na kushindwa kwa staa wao Ronaldo.
Ronaldo
Ronaldo na mtoto wake wakiwa mbele ya sanamu hilo baada ya kulizindua mwaka 2014
Previous Post Next Post