HASSANI KAUNJE AWAHAKIKISHIA WANANCHI WA JIMBO LA LINDI KUWALETEA MAENDELEO KATIKA SEKTA YA KILIMO, ELIMU NA UVUVI

Hassani Kaunje
Katibu wa CCM wilaya ya Lindi Mjini Ndg: Mohamed Kateva akimkabidhi Fomu mgombea Ubunge wa Jimbo la Lindi Mjini Kupitia CCM Ndg Hassani Kaunje. Tukio Hilo lilifanyika Hivi karibuni. 
Hassani Kaunje
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Lindi Mjini Kupitia CCM Ndg Hassani Kaunje(mwenye suruali Nyeusi) akitoka mwenye furaha Mara baada ya Kuchukua Fomu ya Kuwania kiti cha Ubunge wa Jimbo la Lindi Mjini, Tukio hilo limefanyika Hivi Karibuni.

Na. Mwandishi Wetu, Lindi
Mmoja wa makada wa Chama Cha Mapinduzi,anayetarajia kuomba ridhaa ya chama hicho ili awe mgombea wa ubunge katika jimbo la Lindi mjini, Hassan Kaunje. Amesema akichaguliwa nakuwa mbunge wa jimbo hilo atafanya mabadiliko makubwa katika seketa za kilimo, uvuvi na elimu.
Kaunje ambaye alizungumza na mwandishi wa Blog hii hapo jana mjini Lindi. Alisema iwapo chama chake kitamteua kuwa mgombea wake, na wananchi kumchagua, atashirikiana na wananchi wa jimbo la Lindi katika kufanya mabadiliko yenye tija katika sekta za kilimo, uvuvi na elimu.
Alisema kutokana na mahitaji ya kiuchumi kupitia kilimo, wananchi hawanabudi kujikita zaidi katika kilimo cha mazao ya biashara. Ikiwamo kilimo cha mbogamboga na matunda. Alibainisha kuwa soko la mazao hayo ni zuri na litaendelea kuwa zuri kutokana na mahitaji makubwa hasa baada ya ugunduzi wa gesi asilia katika mikoa ya Lindi na Mtwara.
"kuhusu mazao ya chakula, nitahamasisha wananchi kulima mazao yanayostahamili ukame, kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa," alisema Kaunje.
Alisema ili wananchi wawe na uhakika na maeneo yao ya kilimo, kuna umuhimu mkubwa wa wananchi hao kumilikishwa ardhi kwa mujibu wa sheria.
Kuhusu elimu, mtia nia huyo ambaye ametamka wazi kuwa hajachukua fomu ili kushiriki bali kushindana na kushinda. Alisema tatizo la elimu halipo katika vifaa tu, bali hata mtazamo wa jamii kuhusu elimu ni hasi. Hivyo kunahaja ya kuanza kuwekeza kifikra na kimtazamo katika sekta hiyo muhimu kwa maendeleo ya nchi yoyote duniani. 
Aidha Kaunje katika mikakati yake hakuacha kuizungumzia sekta ya uvuvi ambayo pia inatoa ajira kwa wananchi wa jimbo hilo. Ambapo alisema atahakikisha kwa kutumia mfuko wa jimbo, mapatato ya halmashauri na wahisani wavuvi wanapata zana za kisasa za kuvulia na kusafiria ambazo zitawafanya wasafiri umbali mrefu na kufikia maeneo yenye samaki wengi.
"Yote hayo yanaweza kufanikiwa iwapo tutashirikiana na kila mmoja akitimiza wajibu wake kwa kufanya kazi kwa bidii, na kuwa na miradi shirikishi ya kiuchumi ambayo imepangiliwa vema katika mifumo na miundo sahihi," alibainisha Kaunje.
Jimbo la Lindi mjini, lilichukuliwa mwaka 2010 na mgombea kupitia chama cha CUF, Salum Barwany. Ambaye alimshinda aliyekuwa anatetea nafasi hiyo katika uchaguzi huo, Mohamed Abdulaziz wa CCM.
Previous Post Next Post