Unknown Unknown Author
Title: BREAKING NEWS:: WATU 13 WAFARIKI DUNIA KATIKA AJALI MKOANI SINGIDA LEO HII.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
ABIRIA 13 wakiwemo watatu wa familia moja wamefariki dunia mkoani Singida leo, baada ya gari walilokuwa wakisafiria aina ya Noah T.730 BU...
Ajali Mkoa wa singida
ABIRIA 13 wakiwemo watatu wa familia moja wamefariki dunia mkoani Singida leo, baada ya gari walilokuwa wakisafiria aina ya Noah T.730 BUK, kugongwa na Lori aina ya Scania.

Ajali hiyo ya kusikitisha imetokea leo saa 1.32 asubuhi katika barabara kuu ya Singida-Dodoma eneo la kijiji cha Isuna tarafa ya Ikungi wilaya ya Ikungi mkoani Singida.
Ajali Mkoa wa singida
Kamanda wa polisi mkoa wa Singida, SACP , Geofrey Kamwela, amesema gari hilo aina ya Noah lilikuwa likitokea Itigi wilaya ya Manyoni na lilikuwa na safari ya kuja Singida mjini.
Ajali Mkoa wa singida
Amesema hadi sasa miili ya abiria 10 wamekwisha tambuliwa na ndugu zao na miili ya abiria watatu, bado haijatambuliwa na miili yote bado imehifadhiwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya mkoa mjini Singida

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top