Unknown Unknown Author
Title: MDIMU: WANAO UNGA MKONO VITA DHIDI YA MAUAJI YA ALBINO MKONO JUU
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
"Ni kweli mimi ni Albino, nimejikubali na nimeishi maisha yangu yote bila kujali nilivyo. Sijawahi kutumia hali yangu kupata kitu kw...
 Henry Mdimu
"Ni kweli mimi ni Albino, nimejikubali na nimeishi maisha yangu yote bila kujali nilivyo. Sijawahi kutumia hali yangu kupata kitu kwa huruma, nimeyapigania maisha yangu na nimepiga hatua.

Leo hii naongea nanyi nikiwa Baba, Mume, Mwandishi Mwandamizi, Blogger, na mengine mengi, lakini hali yangu sasa inaanza kunikwaza.

Haya mauaji jamani, nimejiteua kuwa Balozi, nitatetea, na kusimama mbele ya wenzangu wote wenye hali kama hii, kama ni wanasiasa ama wafanyabiashara, wanataka kutuua kwa maslahi binafsi, mwaka huu HAPANA.

Wanaoniunga mkono mikono juu"
Mwisho wa kunukuu.

Nikiwa kama Blogger na Mwanahabari, Henry Mdimu aliejitolea kuwa Balozi, nanyoosha mkono juu kwa kuunga mkono kupiga vita vikali mauaji ya ndugu zetu wenye Albinism. kwani wao pia ni Binadamu kama tulivyo mimi na wewe.

LINDIYETU BLOG NA UONGOZI WAKE WOTE UKIONGOZWA NA ABDUL AZIZ UMENYANYUA MIKONO JUU KUUNGANA NAWE ZEE LA NYETI.

JAMANI SASA BASI, NA KILA MMOJA WETU AWE MLINZI KWA NDUGU ZETU HAO.

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top