Picha za wananchi/wanawake wa Mtaa wa Nachingwea uliopo katika Manispaa ya Lindi wakichota maji yanayotoka katika bomba la maji lililopasuka ili kujinusuru na tatizo sugu la uhaba wa maji ya bomba katika maeneo hayo kwa miaka mingi licha ya kuwepo katika makao makuu ya Mkoa wa Lindi.
Wanawake/wananchi hao walichota maji hayo yaliyokuwa yanatiririka ardhini bila kujali yalikuwa safi na salama kwa matumizi ya binadamu ama sio salama wala safi.
Tukio hilo ni jioni ya tarehe 03/01/2015 kama mwanaharakati alivyojionea hali hiyo.
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.