Unknown Unknown Author
Title: ALICHOKISEMA CRISTIANO RONALDO DHIDI YA MCHEZAJI MWENZAKE WA REAL MADRID GARETH BALE HICHI HAPA
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Mwanasoka bora wa dunia kwa mwaka 2014, Cristiano Ronaldo dos Santos Aveiro, amewataka mashabiki wa klabu ya Real Madrid kumuonyesha ushi...
Mwanasoka bora wa dunia kwa mwaka 2014, Cristiano Ronaldo dos Santos Aveiro, amewataka mashabiki wa klabu ya Real Madrid kumuonyesha ushirikiano wa kutosha mshambuliaji wa pembeni kutoka nchini Wales Gareth Frank Bale.

Ronaldo, ametoa wito huo kwa mashabiki wa Real Madrid kwa kuamini Bale bado ana nafasi ya kuendelea kufanya vyema na kufikia hatua ya kuwa mchezaji bora duniani.

Ronaldo amesema Bale tangu alipojiunga na Real Madrid amekua na mchango mkubwa katika kikosi cha The Meringues ambacho kwa mwaka 2014 kilitwaa mataji manne.

Amesema anakumbuka hata yeye aliposajiliwa klabuni hapo mashabiki walionyesha kumkubali na kuendelea kumpa ushirikiano mpaka amefikia hatua ya kuwa mchezaji bora wa dunia, hivyo anaamini nguvu hizo zikielekezwa kwa Bale mambo yatakua mazuri zaidi siku za usoni.


BOFYA PLAY::

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top