Kopunovic amesema hayo jana usiku baada ya mchezo huo kumalika katika Uwanja wa Amani hapa visiwani Zanzibar, ambapo mabingwa hao wa michuano ya tisa ya kombe la mapinduzi walikabidhiwa kikombe chao na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dr. Ally Mohamed Shein.
“Niliamua kumtoa Manyika na kumuingiza Ivo nikijua kabisa huyu ni mkongwe, na anauwezo mkubwa wa kudaka penati, kwahiyo ubingwa huu yeye ndio ameuleta kwani amepangua penati muhimu sana iliyotupatia kombe” Amesema Kopunovic.
IVO NA KOCHA WAKE WAKISHANGILIA USHINDI
Kocha huyo jana alifanya mabadiriko ya kumtoa aliyekuwa kipa wa michuano hiyo toka inaanza Peter Manyika na kumuingiza Ivo Mapunda ambaye hakuwepo toka mwanzo kufatia kuwa katika 40 ya Mama yake, ingawa alirudi na kujiunga na timu katika mchezo wa nusu fainali lakini hakucheza hadi hapo jana ambapo aliibeba Simba katika mikwaju ya penati.
Ubingwa huo unakuwa wa kwanza kwa kocha huyo ambaye bado hajamaliza mwezi akiwa na Simba baada ya kuchukua mikoba ya aliyekuwa kocha wa Simba Mzambia Patrick Phiri ambaye alitimuliwa kufatia matokeo mabaya ya sare.
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.