Happy Birthday Ahmeid Abdullaziz.....
Wikiend hii imekuwa ya furaha kwa kijana Ahmeid ambaye ni mtoto wa kwanza wa Mwandishi wa Channel Ten pamoja na Lindiyetu.com kwa kutimiza miaka 10.
Katika kusherehekea sikukuu yake ya kuzaliwa Kijana huyo aliweza kuwezeshwa na wazazi wake kufurahia kwa pamoja na Marafiki zake wa karibu sherehe fupi iliyofanyika nyumbani kwao Mitaa ya Mikumbi, Lindi Mjini.
Pia kupitia Mtandao wa Kijamii Baba Mzazi alichukua fursa ya kumtakia maisha mema na aliandika ujumbe huu hapa
"
Namshukuru Mungu Mtoto wangu wa kwanza leo amefikisha Miaka 10 toka azaliwe..Inshaallah leo Nimemsomea Dua iliyoambatana na Dua KWA Wazazi wangu wote waliotangulia mbele ya Haki ikiwa pia siku HII ya leo tr 26 sept 2015 ..Inakamilisha Miaka 8 na miezi 6 toka afariki mama yangu mzazi ..TUWAOMBEE DUA..Ameen"
Ahmeid akiwa na wadogo zake nyumbani wakijiandaa kusherehekea siku yake ya kuzaliwa
Ahmeid Akizima Mishumaa
Marafiki na Majirani wa Ahmeid wakiimba wimbo wa Happy Birthday kwa Rafiki yao wakati wa tendo la Kuzima mishumaa....
Ahmeid Akikata keki Baada ya Tendo la Kuzima mishumaa.....
Ahmeid akimlisha keki dada yake ambaye ndio mdogo wake aliyemuachia ziwa.....
Ahmeid akilishwa keki na Mama yake Mzazi
Ahmeid akiwalisha Keki marafiki na Majirani waliohudhuria Sherehe yake ya Kuzaliwa.
Marafiki wa Ahmeid wakiendelea kufurahia sherehe hiyo ya kuzaliwa......
Ahmeid akipokea zawadi kutoka kwa Mdogo wake
Ahmeid akipongezwa na Baba na Mama yake katika siku yake ya kuzaliwa.
Ahmeid akipokea mikono ya Pongezi kwa Marafiki zake waliohudhuria sherehe yake ya kuzaliwa.
Ahmeid akiwa katika picha ya pamoja na wazazi wake na wadogo zake.
Ahmeid akiwa katika picha ya pamoja na Marafiki zake walioweza kuhudhuria sherehe yake ya kuzaliwa.