NICK MINAJ ATAJA SIFA ZA MPENZI ANAEMUHITAJI KWA SASA, HII NI BAADA YA KUACHANA NA SAFAREE SAMUELS

Nick Minaj
Baada ya kutengana na mpenzi wake safaree Samuels,Hitmaker wa nyimbo ya Anaconda Nick Minaj ametaja vigezo vya mpenzi atakayekua naye kwa sasa.

Alisema moja ya vigezo anavyovitaka ni kupata mpenzi atakayekubali umahiri wake katika kazi zake na kuheshimu anachofanya.

“Nataka mwanaume atakayeheshimu na kuthamini uwezo wangu wa kufanya kazi.”alisema Nick Minaj.
Nick Minaj
Rapa huyo mwenye miaka 32 ameamua kuwa wazi baada ya kuvunjika kwa uhusiano wake na mpenzi wake Safaree uliodumu kwa miaka 12 na anahitaji umakini katika ufanyaji wake wa kazi.

Katika majibizano yake na mtangazaji Elliot Wilson alisema “Nimepoteza sehemu kubwa ya maisha yangu kwa kuachana na Safaree na sababu mojawapo nilikua busy zaidi na kazi ”

“Labda wanahitaji uangalizi zaidi na nilikua najali zaidi familia yangu,,sasa ni kazi yangu kuchagua kazi ama mapenzi.”alisema

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post