Unknown Unknown Author
Title: MAMA KIKWETE AWATAKA WAKAZI WA MKOA WA LINDI KUJITOLEA KUCHANGIA MADAWATI ILI KUBORESHA ELIMU YA WATOTO
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Na Anna Nkinda – Maelezo, Lindi Wakazi wa mkoa wa Lindi wametakiwa kuunganisha nguvu zao na kujitolea kuchangia madawati ili kuboresha e...
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete

Na Anna Nkinda – Maelezo, Lindi
Wakazi wa mkoa wa Lindi wametakiwa kuunganisha nguvu zao na kujitolea kuchangia madawati ili kuboresha elimu ya watoto ikiwa ni pamoja na kuimarisha miundombinu na mazingira bora ya kufundishia na kujifunza.

Rai hiyo imetolewa jana na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakati wa hafla fupi ya kukabidhi sampuli za madawati katika shule za msingi kwa ajili ya wanafunzi wa madarasa ya awali kwa uongozi wa Manispaa ya Lindi iliyofanyika katika shule ya Msingi Rahaleo.

Mama Kikwete ambaye ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) alisema mkoa huo umekuwa nyuma kielimu kwa muda mrefu hivyo basi ni jukumu la jamii kushirikiana kwa pamoja na kuwekeza katika elimu ili watoto wapate elimu bora ambayo itawasaidia katika maisha yao.

“Wazazi, walezi na wananchi tunapaswa kuona aibu na kutovumilia kuona wanafunzi wanakaa chini. Hii siyo aibu ya Serikali bali ni aibu yetu sisi wazazi na walezi na viongozi wa Kata na Wilaya”.

"Tatizo la madawati liko ndani ya uwezo wetu hatuwezi kusubiri Serikali kuu hadi watakavyokuwa tayari. Tunachangia maharusi na shughuli nyingine lakini tunashindwa kuchangia kwenye elimu, inasikiisha”, alisema.

Mama Kikwete pia aliwataka viongozi wa mkoa huo kuweka suala la madawati katika vipaumbele vyao kwa muda maalum kwani ukimuandaa mtoto katika umri mdogo na kumjengea mazingira mazuri ya kusoma ikiwa ni pamoja na kukaa katika madawati atapenda shule na hata mwandiko wake utakuwa mzuri.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Lindi Dkt. Nassor Hamid aliwataka walimu wa shule za awali kufanya jitihada na kuhakikisha watoto wanajua kusoma na kuandika kabla hawajaingia darasa la kwanza kwani ni aibu kuona mtoto anaingia darasa la kwanza hajui kusoma wala kuandika.

“Shule za awali ni mahali ambapo vipaji vya watoto vinatambuliwa ni muhimu kwa walimu wakati wanaandika ripoti za wanafunzi kwa wazazi wakaandika na vipaji walivyovitambua kutoka kwa watoto hao hii itasaidia kuviendeleza”, alisema Dkt. Hamid.

Akisoma taarifa ya elimu ya manispaa ya Lindi Hassan Yusufu ambaye ni mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Rahaleo alisema wanafunzi wa madarasa ya awali wanatumia vyumba vya madarasa ya shule za msingi isipokuwa shule ya msingi Mtanda ambayo inavyumba viwili vya madarasa ya awali.

Mwalimu Yusufu alisema, “Wanafunzi wa elimu ya awali kwa kiasi kikubwa wanatumia thamani za shule ya Msingi. Shule chache zina madawati ya wanafunzi wa awali na baadhi ya shule zilipata msaada wa thamani kutoka kwako Mama Kikwete tunashukuru sana. Msaada huu umekuwa na manufaa sana kwetu katika kujenga misingi imara ya wanafunzi”.

Mwalimu huyo alisema mahitaji ya madawati katika manispaa hiyo ni 752 kwa shule za awali yaliyopo ni 448 na kwa shule za msingi ni madawati 3,994 yaliyopo ni 3,537 hivyo kuwa na upungufu wa madawati 304 kwa shule za msingi na 699 kwa shule za awali.

Halmashauri ya Manispaa ya Lindi ina jumla ya shule za msingi 32 kati ya hizo za Serikali ni 31 ambazo zote zina madarasa ya awali na moja ya binafsiKatika madarasa ya awali kuna jumla ya wanafunzi 1803 kati ya hao wavulana 920 na wasichana 883.

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top