Kamanda wa polisi Mkoa wa Lindi Renata Mzinga
"Taarifa ya kutupwa kwa kichanga huyu zimepatikana kupitia kwa mtendaji wa kata hiyo, Msafiri Wanie, baada ya kupewa taarifa kuwa mwanamke huyo amemtupa kitoto chake chenye umri wa siku moja"Alisema Mzinga.
Mzinga amewaambia waandishi kuwa baada ya kuokotwa kwa mtoto huyo na kufanyiwa uchunguzi na Daktari wa kituo cha Afya kata ya Rondo alibainika alikuwa tayari ameshakufa.
Amesema tayari mwanamke huyo anashikiliwa na Polisi na katika mahojiano amesema alichukuwa uwamuzi wa kumtupa kichanga chake kutokana ugumu wa maisha, ikiwemo mwanaume aliyezaa naye kukataa kumsaidia katika matunzo yake.
Kamanda huyo wa Polisi mkoani Lindi, amesema mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani mara baada ya kukamilisha upelelezi na taratibu za kiofisi, kujibu shitaka linalomkabiri la mauaji.
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.