Unknown Unknown Author
Title: KILWA WAENDELEA KUNUFAIKA NA UWEKEZAJI WA GESI.
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Na Abdulaziz Kilwa Masoko Wananchi  wilayani Kilwa mkoani Lindi wameendelea kunufaika na wawekezaji,baada ya kampuni ya uchimbaji gesi y...
zahanati ya kijiji cha Nangurukuru
Na Abdulaziz Kilwa Masoko
Wananchi  wilayani Kilwa mkoani Lindi wameendelea kunufaika na wawekezaji,baada ya kampuni ya uchimbaji gesi ya PANAFRICAN ENERGY kuikabidhi halmashauri  hiyo zahanati ya kijiji cha Nangurukuru ambayo ujenzi wake umegharimu Tshs 262 Milioni .


Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo ambayo yalifuatiwa na utiaji sahihi mkataba wa ujenzi wa nyumba mbili za watumishi wa zahanati hiyo ambazo ujenzi wake hadi kukamilika utagharimu shilingi 458 milioni.

zahanati ya kijiji cha Nangurukuru

Meneja wa huduma za jamii wa kampuni hiyo, Andrew Kashangaki alisema katika ujenzi wa zahanati hiyo kampuni ya PANAFRICAN ENERGY imechangia jumla ya shilingi 216,000,000 Ambapo pia kutokana na tatizo la wafanyakazi pia kampuni imeamua  kufadhili ujenzi wa nyumba mbili za watumishi wa zahanati hiyo ambazo mkataba wenye thamani ya shilingi 458,000,000 ulisainiwa baina ya mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo Bw David Roberts na Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Kilwa katika hafla hiyo fpi ya kukabidhi zahanati.
zahanati ya kijiji cha Nangurukuru

Aidha Kashangaki alibainisha kuwa  sera ya kampuni hiyo licha ya kufanya kazi ya uzalishaji wa Gesi ya songosongo pia hutoa  misaada kwa jamii ikiwemo kufadhili programu ya ufundishaji lugha ya kiingereza kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza wa shule za sekondari za halmashauri hiyo, ambapo jumla ya shule za sekondari 20 kati ya 28 zimenufaika na programu hiyo.

"Wana kilwa  tulianza kusaidia elimu ya kiingereza kwa kuzifikia shule 20 ila kwa umuhimu wa elimu kuanzia mwakani tutazifikia shule zote 28 za sekondari ikiwemo kusaidia upatikanaji wa Umeme Jua kwa shule ambazo hazina umeme" Alimalizia Kashangaki

zahanati ya kijiji cha Nangurukuru
Mkuu wa wilaya Ya Kilwa, Abdallah Ulega licha ya kuishukuru kampuni hiyo aliwataka wananchi kupuuza kauli zinazosemwa ikiwemo baadhi ya Vyombo vya habari kupotosha na kudai Manufaa ya Gesi yapo katika kijiji cha Songosongo  pekee Na kubainisha baadhi ya maeneo yanayonufaika ikiwemo hapo Nangurukuru, Njinjo, Somanga na kilwa masoko
"Wananchi wa Kilwa nadhani ni mashahidi kampuni hii imesaidia wilaya yote si Kama Gazeti moja lilivyoandika hivi karibuni Huu ni upotoshaji mkubwa kwani elimu inasaidiwa wilaya yote, Afya Hivyo hivyo, Maji wananufaika mpaka Njinjo na hata mrahaba unaolipwa na kampuni hiyo zaidi ya Nusu inachangia katika sekta ya elimu Tuwe makini kuyajuahaya yenye ukweli si maneno tu ya vijiweni..." Alimalizia Ulega
zahanati ya kijiji cha Nangurukuru
Awali akifungua hafla hiyo Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Nangukuru, Hamis Ligweje alisema kabla ya PANAFRICAN kufadhili ujenzi huo, wananchi wa kijiji hicho kwa kushirikiana na wahisani wengine ikiwamo  shirika la Action Aid walichangia walichangia jumla ya shilingi  Milion 46 ujenzi  ambao ulikuwa wa kusuasua mpaka wahisani hao walipojitokeza kusaidia kuikamilisha.

"Hakika tulishindwa kabisa na Tulifikia hatua ya Kumuomba Rais Kikwete Kusaidia alipokuja katika ziara yake ambapo aliwaagiza Viongozi wa Wilaya kuangalia uwezekano ndipo Mkurugenzi aliehama Bw Mapunda Alifanikisha kuwaomba hawa wahisani na leo wametukamilishia na tunafarijika zaidi walipoamua kutujengea na Nyumba 2 kwa 4 za watumishi itasaidia sana si kwa Nangurukuru tu hata wasafiri watakaopata dharula katika barabara kuu"

zahanati ya kijiji cha Nangurukuru
Licha ya kukabidhi Zahanati hiyo Mkurugenzi mkuu wa Pan African Energy, David Roberts Alikabidhi Vitanda Viwili vya kujifungulia akina mama ikiwa ni hatua ya awali ya kuokoa Akina mama katika suala la Uzazi

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top