MOTO WATEKETEZA NYUMBA ENEO LA MWANANYAMALA JIJINI DAR LEO

moto mwananyamala
Gari ya Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji likiwa eneo la Mwanyamala mapema leo mchana,ambapo moto mkubwa umezuka na kuteketeza nyumba nzima na mali zilizokuwemo,ambazo thamani yake haikujulikana mapema,tukio hilo limetokea maeneo ya Mwananyamala jirani na hospitali ya Mwananyamala.
moto mwananyamala
Baadhi ya watu wakishuhudia tukio la Moto lililotokea mapema leo mchana,ambapo moto huo umeteketeza nyumba nzima na mali zilizokuwemo,ambazo thamani yake mpaka Globu ya jamii inaondoka eneo la tukio haikufahamika.
moto mwananyamala
Baadhi ya Askari wa Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji wakiendelea kuzima moto kwenye moja ya chumba cha nyumba hiyo,Mashuhuda waliokuweo kwenye tukio hilo wanaeleza kuwa chanzo cha moto huo ni hitilafu ya umeme iliyokuwa imetokea kwenye moja ya chumba ndani ya nyumba hiyo.
moto mwananyamala
Majirani walijitokeza kuzima moto kwa kutumia ndoo kama uonavyo pichani
moto mwananyamala
Mabati yaliyobahatika kutetekea kwa moto yakitolewa nje.
moto mwananyamala
Askari wa Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji wakiendelea kuzima moto.
moto mwananyamala
Baadhi ya raia wema pia walijitokeza kusaidia kuuzima moto huo.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post