YANGA YAICHAZARA BILA HURUMA KOMOROZINE DE DOMONI GOLI 7–0 UWANJA WA TAIFA

clip_image002[5]Mshambuliaji wa Timu ya Yanga,Hamis Kiiza akiipachikia timu yake bao la nne kati ya saba yaliyotiwa kimiani wakati wa mchezo wao wa Klabu Bingwa Barani Afrika uliochezwa hivi leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Yanga imeshinda kwa Bao 7-0.Mshambuliaji wa Yanga,Mrisho Ngassa akiondoka na mpira huku mabeki wa timu ya Komorozine ya nchini Comoro wakimsindikiza wakati wa mchezo wao wa Klabu Bingwa Barani Afrika uliochezwa hivi leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Yanga imeshinda kwa Bao 7-0.Mrisho Ngassa bado yuko na mpiraaaaa.....Mrisho Ngassa anapachika bao paleeeee...... Gooooooooo ni goli la sita hili lililofungwa na Mrisho Ngassa na kuwa mchezaji pekee aliefunga bao tatu peke yake.Wachezaji wa timu ya Komorozine wakilaumiana.

Mabingwa wa Tanzania, Yanga wameitembezea kipigo cha mbwa mwizi timu ya Komorozine de Domoni toka Comoro cha mabao 7-0. Mabao ya Yanga yametiwa kimiani na Mrisho Ngassa (13,65,68), Didier Kavumbagu (58,81), Cannavaro (20) na Hamis Kiiza (59).

Hongera sana Dar es Salaam Young Africans.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post