Unknown Unknown Author
Title: LIVE: UCHAGUZI MDOGO WA MADIWANI KATA 27, TUTAWALETEA KILA KINACHOTOKEA
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Tanzania. kama kawaida, leo Tutakuletea mwenendo mzima wa uchaguzi wa udiwani katika kata 27 nchini ambapo wananchi watapiga kura kuwachagu...

KURATanzania. kama kawaida, leo Tutakuletea mwenendo mzima wa uchaguzi wa udiwani katika kata 27 nchini ambapo wananchi watapiga kura kuwachagua madiwani wao kwenye kata hizo.

Tutawaletea matukio kwenye kata hizo, hasa Kata ya Sombetini ambayo imevuta hisia za watu wengi kutokana na kata hiyo kuwa katika mkoa wenye ushindani mkubwa wa kisiasa.

Pia matokeo ya kura, kama vurugu zitatokea au kuibwa kwa kura- yote hayo tutawajulisha kupitia lindiyetu.com.

Updates


Mbunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ashambuliwa, L. Mwanjali Mbeya Vijijini apigwa na kujeruhiwa asubuhi hii kwenye uchaguzi kata ya Santilya, polisi yakamata 7 wa Chadema kuhusika.

Source; Mwananchi BreakingNews.

Updateslindi leo 9

Kata ya Kiwalala Mjini Lindi, Wananchi wameendelea na Zoezi la Upigaji kura kwa hali ya Usalama na Kufuata taratibu zote zilizowekwa na Tume ya uchaguzi, Hakuna Tatizo lililojitokeza hadi Sasa

Updates Arushaclip_image001Mmoja ya wapiga kura katika Kata ya Sombetini Arusha, akivutana na polisi HIVI PUNDE baada ya kutimiza haki yake. Polisi walikuwa wanamtaka akae mbali na eneo la kupigia kura.

UPDATES

clip_image001[1]

WAKATI Chama Cha Mapinduki (CCM),ikishinda Kata 24 Kati ya Kata 27 ambazo Uchaguzi Mdogo wa Madiwani Umefanyika jana Kote Nchini, mjini Kigoma katika jimbo la Mbunge wa Chadema Zitto Kabwe ushindi umekwenda kwa CCM.

Hatua ya Chadema kushindwa katika kata ya Mkongoro inatokana na  mgogoro ulioikumba Chama hicho baada ya Mbunge huyo kuvuliwa nyadhifa zake   ndani ya chama hicho.

Mchanganuo  wa  matokeo  hayo  katika baadhi ya kata  kwa  ufupi

KUTOKA BAGAMOYO KIBINDU. Matokeo ya jumla: CCM- kura 1682(75%),CHADEMA- kura 548(25%).

MAGOMENI :Matokeo kwa jumla: CCM 1183, CUF 708, CHADEMA 347.

KUTOKA LINDI NA MTWARA. CCM imeshinda Kata Zote za Uchaguzi Uliofanyika  jana .

NACHINGWEA. ...ADC -9 CUF -110 CHADEMA -188 CCM -517.

KUTOKA KIGOMA JIMBONI KWA ZITTO KABWE: CHADEMA wamepoteza kata ya  MKONGORO Jimboni KWA Zitto Kabwe,Imechukuliwa na CCM(Kata Ilikuwa  Inaongozwa na CHADEMA).

KUTOKA MOSHI.  Kata ya Kiboroloni imebakia  CHADEMA

KUTOKA KONDOA: CCM --1,296  CUF--935. CDM--29 NCCR—34

KUTOKA SOMBETINI JIJINI ARUSHA: CHADEMA Imeshinda Kata ya Sombetini  kwa 2548 na CCM 2077

KUTOKA RUNGWE MKOANI MBEYA: CCM Imeshinda kata ya  Malindo na Matokeo rasmi Kata ya SANTILYA-Mbeya Vijijini. CCM - 1650 CDM - 1154.

KUTOKA MANYARA KITETO: CCM Imeshinda kata Zote mbili ikiwamo ya  Partimbo.

KUTOKA KAHAMA KIBAGWE: CCM Imeshinda Kata ya Kibagwe (kulikuwa na Kata  moja tu ya Uchaguzi).

KUTOKA BUNDA: CCM Imeshinda (Kulikuwa na Kata Moja  ya Uchaguzi)

KUTOKA NJOMBE MJINI:: Chadema Imeshinda ( Kata Ilikuwa Moja  tu ya Uchaguzi).

KUTOKA LUDEWA :CCM imeshinda,Kulikuwa na Kata Moja ya  Uchaguzi.

Hitimisho: Katika kata 27 zilizofanyiwa Uchaguzi,CCM Imeshinda kata 24,Chadema Kata 3. Kwa Maana hiyo CCM Imeshinda Kwa Kishindo Uchaguzi huu hasa Ukizingatia  UShindani wa Kisiasa Uliokuwepo siku za  hivi Karibuni..

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top