HATIMAE ILE KERO YA SHIMO ENEO LA SOKO KUU LINDI IMEPATIWA UFUMBUZI

clip_image001Hatimaye Shimo lazibwa jana na Kampuni ya simu Tanzania.....

Na Abdulaziz, Lindi

Mtandao huu ulilipoti shimo lililokuwa katika eneo la soko kuu Mjini Lindi kuwa ni kero kwa watumiaji wa Barabara hiyo kwani huwa inaleta ajali mbalimbali hatimae shimo hilo limezibwa jana na Kampuni ya simu Tanzania. (Kama hukusoma bofya hapa)clip_image001[6]Chakusikitisha nilipoenda leo kupiga picha shimo likiwa limezibwa baadhi ya Vijana walinifukiza na kuropoka kuwa Picha zangu zimezuia ulaji wao kwa kuwa ni magari mengi na bajaj zilikuwa zikitumbukia na wao kufaidika kwa kupata chochote kitu siku zinaenda......

Je tutafika kweli? na Je tuache kufichua kwa ajili ya maendeleo ya Jamii yetu? Hebu Tuambie mdau wetu

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post