ANGALIA PICHA MBALIMBALI ZA SHEREHE YA PARIS CLUB YA KUTIMIZA MWAKA 1 WA BURUDANI

DSC06199Wachezaji wakiingia uwanjani ilikuendelea na Mechi iliyochezwa siku ya Jumamosi uwanja wa Ilulu katika Bonanza la Paris ClubDSC06200Benchi la Ufundi la Timu ya Mashabiki wa Simba walioibuka washindi katika Mechi hiyo

Paris Club, Club ya Burudani ndani ya Lindi imetimiza mwaka mmoja wa Burudani ndani ya Manispaa ya Lindi. katika kusherehekea siku hiyo Club hiyo imewaalika wadau wake wote wa mji huu kushiriki katika michezo mbali mbali ikiwa ni kukimbiza kuku na kuvuta kamba pamoja na michezo ya mpira, ikiiwa ni kwa upande wa wasichana na wavulana hao wote wakiwa katika makundi mawili nayo ni mashabiki wa Simba na Yanga.

DSC06209Wachezaji wa Timu ya Mashabiki wa Yanga wakisubiri uamuzi wa Waendesha mashindano kuongezwa dakika au kupigwa penalt baada ya kutoak suruhu 2 – 2.

Mashabiki wa Yanga kwa upande wa wanawake waliibuka mabingwa katika mchezo wa netball, kwa upande wa wanaume washabiki wa Simba walitawazwa mabingwa kwa sababu Mashabiki wa timu ya Yanga Kugomea kuendelea kucheza dakika za Nyongeza mara baada ya Dakika za Kawaida kuisha na matokeo kuwa Ni Bao 2 – 2.

Mashabiki wa Yanga waligomea mchezo huo wa kuongeza dakika kwa kile kilichosemwa kuwa wamecheza katika jua kali na tayari wamekwisha choka hivyo walitaka zipigwe Penalt tu,

DSC06213Uongozi wa waendesha mashindano katika Bonanza hilo kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Paris Club ndg Saidi Matengula, Salma VaaDude, Segesela.

Lakini Viongozi walioandaa mashindano hayo ilionesha dhahili kuwa walikuwa wapenzi wa timu ya mashabiki wa simba kwakile kilichoonekana kiwanjani hapo kwa kuamrisha ziongezwe dakika thelathini na kuruhusu timi ya Mashabiki wa simba kubadilisha timu nzima na kuingiza wachezaji wapya huku wakijua kuwa timu ya Yanga walikuwa hawana wachezaji wa Akiba na kujua lazima watawafunga kwa jinsi walivyokuwa wamechoka.

Hivyo waliamua kugoma na kutoingia uwanjani na kufanya kupatikana ushindi kwa Timu ya Mashabiki wa Simba.

**********************************************

USIKU ILIKUWA NI BIRTHDAY PARTY NA WATU WALIFURIKA KUSHEREHEKEA PARTY HIYO CHEKI PICHA BAADHI YA MATUKIO

DSC06290Mgeni rasmi akikuwa ni Kaimu mkurugenzi wa Manispaa ya Lindi ambae ni wa tatu kutoka kulia akiwa na mkurugenzi wa Paris Club na wageni waalikwaDSC06215Wanakamati wa sherehe wakiwa katika furaha wakati sherehe hiyo ikiendelea katika viwanja vya eneo la club hiyo.DSC06218Wadau wakitokelezea na Camera ya Lindi yetu iliyokuwepo eneo hilo, kushoto ni (Husna Shop na Salma VaaDude)DSC06226Mc aliyeongoza Sherehe nzima kwa jina ULEDIDSC06227Mdau mkubwa wa Paris Club Ndg: Mnonjela nae akiwa na Mkewe alikuwepo kama mgeni mwaalikwa.DSC06237Mr and Mrs Said Matengula Mkurugenzi wa Paris Club akiwa na familia yake katika kusherehekea mwaka Mmoja wa Burudani(Paris Club)shampengShangpen zilifunguliwa………DSC06308Keki ilikatwa pia……..DSC06310

DSC06313

DSC06322Mgeni rasmi akilishwa keki na Mrs Paris ClubDSC06229Mrs Paris Club akiwa mwenye furaha katika sherehe hiyo….DSC06230Mdau mkubwa wa Paris Club ndg Hassani Mnyaya akiwa na Mdau mwenzakeDSC06295Wadau wakiendelea kuburudika na kujiachia na Camera Yetuwadau

DSC06332Mr VaaDude wakwanza kushoto akiwa na wadau wenzakeDSC06234Hadija Mkadamu akiwa ndani ya viwanja hivyo tayari kusherehekea Mwaka mmoja wa Burudani ndani ya Viwanja vya Paris clubDSC06261Wadau wanguvu wakiendelea kusherehekea tafrija hiyo….DSC06262Mr and Mrs Sule nao walikuwepo katika kujumuika na ndugu jamaa na marafiki katika usiku huo wa kutimiza mwaka mmoja wa burudani wa Paris Club.DSC06271Baadhi ya wafanyakazi wa Paris Club wakiwa katika picha Kutoka kushoto ni Dada Mwana na Dullah KibajajiDSC06243Hakika ilikuwa party ya aina yake kwani hakuachwa mtu katika kula au kunywa hata wale waliojitokeza kwa kutochangia waliburudika vilivyo.DSC06334Tyme ya Misosi kama kawa watu walijukuika katika kujipatia milo waitakayoDSC06337

DSC06339

DSC06340

DSC06342

DSC06275Wanakamati walioandaa sherehe hiyo wakiwa katika picha ya pamojaDSC06345Usafiri ulikuwepo masaa yote ila duh madereva waliuchapa usingizi kama mmoja wa madereva boda boda aonekanavyo hapo juu katika pichaDSC06347

Picha zote na Kilozo FS

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post