DC MWANZIVA ATANGAZA MAFANIKIO KATIKA SEKTA YA ELIMU

Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Victoria Mwanziva, ametangaza mafanikio makubwa yaliyopatikana kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanyika katika sekta ya elimu ndani ya halmashauri za Manispaa ya Lindi na Mtama, mkoa wa Lindi. Amebainisha kuwa uwekezaji huo umekuwa na mchango mkubwa katika kuboresha ufaulu wa wanafunzi.

Akizungumza ofisini kwake, Mwanziva alisema kuwa juhudi mbalimbali zinafanywa ili kuhakikisha watoto wa kike wanapewa kinga dhidi ya ukatili wa kijinsia, ili waweze kufikia malengo yao na kuleta mabadiliko chanya katika jamii.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post