MAMA WA JOHN TERRY AKESHA BAA

clip_image001LONDON, ENGLAND

MAMA mzazi wa beki wa kati wa Chelsea, John Terry, Sue, amekutwa akiwa amelewa chakari na kuuchapa usingizi katika siti ya nyuma ya teksi aliyokodi baada ya kuzidiwa na pombe alizokunywa usiku kucha katika baa moja jijini London.

Mama huyo mwenye umri wa miaka 55, alipanda ndani ya teksi hiyo saa 9 za alfariji akiwa ametoka kuponda raha na mkwewe, mke wa Terry, Toni.

Kwenye teksi hiyo, bibi Sue alitangulia kupanda na kwa sababu alichoka, aliamua kuangusha usingizi katika siti ya nyuma akimsubiri Toni atoke ili warudi nyumbani.

Tukio hilo la ulevi wa mama huyo, limekuja siku chache baada ya baba mzazi wa mwanasoka huyo kupandishwa kizimbani kwa tuhuma za ubaguzi.

SOURCE: MWANASPOTI

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post