Unknown Unknown Author
Title: BARCELONA YATAKA KUMSAJILI TORRES AWE SUPER SUB CAMP NOU
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Soma yote juu ya hii: Gazeti la michezo la kila siku la Catalan,  Sport  limeandika kwamba Barcelona inataka kumnunua kwa Euro Milioni 20 To...

clip_image001Soma yote juu ya hii: Gazeti la michezo la kila siku la Catalan,  Sport  limeandika kwamba Barcelona inataka kumnunua kwa Euro Milioni 20 Torres

HAWATOSHI Messi na Neymar peke yao kuongoza safu ya ushambuliaji, Barcelona imeripotiwa kutaka kumnunua mshambuliaji Fernando Torres.

Gazeti la kila siku la Catalan, Sport limeandika kwamba Barcelona inataka kutoa Pauni Milioni 17 (zaidi ya Euro Milioni 20) kumnunua mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 29 anayekipiga Chelsea.

Msimu Mabao
2012-13 22
2011-12 11
2010-11 10
2009-10 22
2008-09 17
Pamoja na hayo, Torres hatakuwa mchezaji wa kikosi cha kwanza bali atakuwa anatokea benchi kama super-sub.
Matumani ni kwamba, Torres atatengeneza uzito sawa na aliokuwa nao Henrik Larsson, ambaye alikuwa kipenzi cha mashabiki enzia zake Nou Camp kwa kufanya vitu adimu akitokea benchi hususan alipotoa pasi za mabao yote Barcelona ikishinda 2-1 dhidi ya Arsenal katika Fainali ya Ligi ya Mabingwa mwaka 2006.
Lakini Sport limemsifia Torres ni mshambuliaji wa uhakika ambaye anaweza kufunga mabao kati ya 20 na 25 kwa mwaka.

Glory goal: Torres scored against Barcelona at the Nou Camp in the Champions League semi-finals last year 

 

Bao la ushindi: Torres alifunga dhidi ya Barcelona Uwanja wa Nou Camp katika Nusu Fainali ya Mabingwa mwaka jana

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top