BARAZA LA IDD KUFANYIKA SONGEA MKOANI RUVUMA

Swala ya Eid El Fitr na Baraza la Eid kitaifa mwaka huu vitafanyika Masjid L-huda Msikiti wa Bakwata Songea katika Mkoa wa Ruvuma.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Waislam Tanzania Suleiman Lolila, Swala hiyo itafanyika kati ya tarehe 19 au 20 Agosti, 2012 kutegemea mwandamo wa mwezi.

Taarifa hiyo imefafanua kuwa Baraza la Eid litafanyika kati ya tarehe hizo hizo kuanzaia saa kumi kamili alasiri.

Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe. Said Mwambungu.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post