POGBA, FRYERS MASAA 48 KUSAIN MKATABA MPYA LASIVYO OUT-MAN UNITED

image

Wachezaji wawili wanaoweka ngumu kusaini mkataba mpya ndani ya klabu ya Manchester United Paul Pogba na Ezekiel Fryers wameambiwa wasaini mikataba mipya ndani ya masaa 48 au wasahau kuichezea tena Manchester United.

Teenagers hao wanaonekana kutaka kufuata mfano wa bad-boy Ravel Morrison nje ya Old Trafford  baada ya kukataa kuweka saini kwenye mikataba mipya kwa muda mrefu sasa.

Pogba 18, na Fryers 19, wanamaliza mikataba yao mwezi June mwaka huu na baada ya kubembelezwa sana sasa inaonekana mabosi wa United wamepoteza uvumilivu na kuawaambia ijumaa ndio mwisho na hatma yao wataichagua siku hiyo.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post