MBUNGE WA JIMBO LA MCHINGA ACHANGIA MILIONI 27

MBUNGE wajimbo la Mchinga mkoani Lindi Saidi Mtanda amechangia miradi ya mbalimbali  ya maendeleo yenye thamani ya shs milioni 27 ikiwamo kuwapa motisha walimu wanaofundisha wilayani humo
DSC00509
Akizungumza na timu ya waandishi habari Mtanda alisema kuwa jimbo la mchinga katika mwaka wa fedha 2011/12 limepokea jumla ya shs milioni 35 na kuzigawa shs milion 27 kwenye miradi mbalimbali ya maendeleoeo jimboni humo.
Mtanda alisema sehemu ya matumizi ya fedha yataelekezwa kulipa ada za wanafunzi zaidi ya 2700 wasio na Uwezo wa kutoka shule za sekondari Mipingo, Kitomanga, Mvuleni, Mchinga, Rutamba, Milola na Nangaru, pamoja na kuwapa motisha walimu wanaojitolea kufundisha shule za awali wilayani humo
Alisema fedha zingine zitatumika kwa ajili ya kufanya utafiti wa maji kwenye vijiji vyenye matatizo,, ukarabati wa nyumba za walimu ujenzi wa madarasa, zahanati, na kusaidia vikundi vya uzalishaji mali vya vijana na Wanawake.
Kutokana mchango Mtanda amewataka wananchi wa jimbo hilo kutumia vyema frusa hizo zilizopatika ili ziweze kuleta tija na kuwaomba kuwapeleka shule Watoto waliochaguliwa kujiunga na kidoto cha kwanza mwaka huu.
Alisema kuwa vyema wazazi na walezi wakaona umuhimu wa kuwapeleka Watoto waliofaulu shule kwa wakati bila kushurutishwa ili kuwaandalia maisha mema ya baadaye pia amewata wadau wengine ndani na nje ya jimboni hilo kuangalia uwezekano wa kuchangia maendeleo katika sekta ya elimu na huduma zingine za kijamii.

Imeandikwa na
Mwanja Ibadi Lindi

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post