Eneo hili lilikuwa limejengwa nyumba, hii ni kutimiza kauli ya Waziri wa wizara ya Ujenzi Mh.Pombe Magufuli ya kuzitaka nyumba zote zilizoko kwenye Road reserve ziondolewe na wananchi wa mnazi mmoja wameitikia wito huo kwa kuanza kubomoa wenyewe kabla halija pita bomoa bomoa.
Nadhani huu ni mwanzo mzuri kwa wananchi hawa na nimatumaini yangu na wengine watafuata mkondo huu kwani ni vyema kutekeleza kabla hujapata hasara na usumbufu mkubwa hapo baadae
