NIJUZE NIJUZE Author
Title: YST INAWASAIDIA WANAFUNZI KUWA WABUNIFU
Author: NIJUZE
Rating 5 of 5 Des:
Dr. Gozbert Kamugisha ambaye ni Mwanzilishi Mwenza wa Taasisi ya Wanasayansi Chipukizi (Young Scientist Tanzania YST) akitoa hotuba wakati w...
Dr. Gozbert Kamugisha ambaye ni Mwanzilishi Mwenza wa Taasisi ya Wanasayansi Chipukizi (Young Scientist Tanzania YST) akitoa hotuba wakati wa utoaji tuzo.

Msomisi Mbenna Mshauri wa Masuala ya Kijamii kutoka Kampuni ya Shell Tanzania

Wanafunzi washiriki katika tafiti mbalimbali kwenye picha ya pamoja na Mgeni Rasmi Viongozi na mfadhili wa Mradi wa YST

Na. Fungwa Kilozo, Lindi

Taasisi ya Wanasayansi Chipukizi Tanzania (YST) Young Scientists Tanzania imekuwa Taasisi iliyojikita katika kuhamasisha na kukuza maendeleo ya Sayansi na Teknolojia kwa wanafunzi wa shule za sekondari nchini kupitia mradi wa kuwajengea uwezo na ujuzi wanafunzi wa sekondari kwenye masomo ya sayansi nchini.

Tangu mwaka 2013 kampuni ya Shell Tanzania wamefadhiri Mradi huo wa kuwajengea uwezo na ujuzi wanafunzi wa Sekondari kwenye masomo ya sayansi nchini unaotekelezwa na YST ili kuboresha sayansi katika shule za sekondari.

Mradi huo Umewawezesha wanafunzi hao kuwa Wabunifu na utamaduni wa kufanya tafiti ambazo zinakuwa na manufaa katika jamii zao na Taifa kwa ujumla.

Hayo yamebainishwa na Bi. Msomisi Mbenna ambaye ni Mshauri wa masuala ya kijamii kutoka kampuni ya Shell Tanzania ambayo ni mfadhili wa mradi huo wakati wa sherehe za utoaji wa tuzo kwa wanafunzi waliofanya vizuri katika tafiti zao mwaka 2023 zilizofanyika Wama-Sharaf Manispaa ya Lindi, ambapo shule mbili zitauwakilisha mkoa wa lindi katika Mashindano ya kitaifa Jijini Dar es Salaam.

Shule 15 za Sekondari za mkoani wa Lindi zimeshiriki katika kufanya tafiti mbalimbali. Shule zilizopata nafasi mbili za juu za kwenda kuwakilisha mkoa kwenye mashindano ya Kitaifa yatakayofanyika Dar es Salaam ni Kivinje Sekondari ya wilayani kilwa na Nkowe Sekondari ya Halmashauri ya Ruangwa ambayo ndio ilikua namba moja.

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top