MRITHI WA KANUMBA ATOA MAJIBU HAYA KUHUSU ELIZABETH MICHAEL (LULU)

KUTOKANA na hivi karibuni mama wa aliyekuwa staa mkubwa wa filamu, Steven Kanumba, Flora Mtegoa kumwanika kijana ambaye ni mwigizaji wa tamthilia, Fredy Swai kuwa ndiye mrithi wa mwanaye, kijana huyo alibadilika muonekano usoni baada ya Global TV Online kumhoji kuhusu ukaribu wake na Elizabeth Michael ‘Lulu’ aliyekuwa mpenzi wa Kanumba.
Fredy Swai na Elizabeth Michael ‘Lulu’
Fredy aliulizwa kama ana mawasiliano na Lulu, alipatwa kigugumizi na kosa jibu la moja kwa moja na alijibu tofuti na swali lilivyomtaka kujibu, katika hali ya kujilazimisha alijibu kuwa hana namba ya Lulu huku akionesha hali ya kukosa amani.

Bado haijafahamika kwa nini alisita kiasi cha kushindwa kujibu ndiyo ndio ua hapana na badala yake akakausha kwanza, baadaye akatoa maelezo.

Akizungumza na Global Tv Online, Fredy alisema hana namba ya Lulu na hajawahi kukutana na Lulu na endapo atakutana nae ataongelea kazi tu kwani amekuwa akizifuatilia sana kazi zake na si vinginevyo.

Saalum Milongo/GPL

++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
KUWA KARIBU NASI LINDIYETU.COM
Usipitwe!! Ungana na Familia hii kupitia FacebookTwitter na Instagram ili kupata Infortainment zote!! Usikose kujiunga na Youtube channel yetu ili kupata Exclusive mbalimbali kali kutoka LindiYetu TV

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post