TRA KWENYE KASHFA YA STIKA ZA KAZI ZA WASANII NCHINI, ALEX MSAMA AWAFICHUA WAUZAJI (+VIDEO)

Alex Msama
Mkurugenzi wa Msama Promotion, Alex Msama

Kampuni ya Msama Promotions imeeleza kuwabaini maafisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA wanaouza stika halisi za mamlaka hiyo kwa ajili ya kutumika kuuzia bidhaa bandia, ikiwemo kazi feki za sanaa.

Hatua hiyo imekuja ikiwa ni siku mbili baada ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo nchini Tanzania Mh. Nape Nnauye kutembelea maduka ya kazi za sanaa katika soko la Kariakoo jijini Dar es salaam na kubaini wauzaji wa kazi feki za sanaa.

Akizungumza leo jijini Dar es salaam mkurugenzi wa kampuni hiyo Alex Msama amesema kuwa suala hilo ni sehemu ya jitihada za kuunga mkono ukomeshwaji wa wahujumu uchumi na wakwepa kodi nchini Tanzania.

Aidha Msama amempongeza waziri Nape na kusema kuwa ni vyema watanzania wakafahamu kuwa kinachohitajika sasa ni watu kufanya kazi halali na sio kuwaibia wengine kwa njia tofauti tofauti.

Msikilize hapa chini akielezea.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post