
Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiagana na Mama Maria Nyerere, Mjane wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, na wanafamilia alipokwenda nyumbani kwake Msasani kumfariji kufuatia kifo cha mkwe wake Marehemu Leticia Nyerere huko Maryland, Marekani.
Leticia Nyerere(Enzi za uhai wake)
Msiba upo DMV 9004 Brightlea Court, Lanham, MD 20706.
Leticia aliolewa kisha kutengana na mtoto wa Hayati Baba wa Taifa, Madaraka Nyerere mwaka 1996, ambapo walifanikiwa kupata watoto watatu.
Leticia alikuwa mtoto wa Mzee Musobi Mageni. Julai 27 2015, Leticia alitangaza kuihama CHADEMA na kurejea Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Mungu ailaze roho ua Marehemu mahali pema, Amina.
Tags
HABARI ZA KITAIFA