RAIS DKT JOHN POMBE MAGUFULI AMFARIJI MAMA MARIA NYERERE, MSIBA WA MKWE WAKE LETICIA NYERERE

Dkt John Pombe Joseph Magufuli
Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiagana na Mama Maria Nyerere, Mjane wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, na wanafamilia alipokwenda nyumbani kwake Msasani kumfariji kufuatia kifo cha mkwe wake Marehemu Leticia Nyerere huko Maryland, Marekani.
Leticia Nyerere
Leticia Nyerere(Enzi za uhai wake)
Aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Leticia Nyerere amefariki dunia katika hospitali ya Doctors Community iliyopo Lan ham, Maryland jana saa mbili usiku kwa saa za Afrika Mashariki.
Msiba upo DMV 9004 Brightlea Court, Lanham, MD 20706.

Leticia aliolewa kisha kutengana na mtoto wa Hayati Baba wa Taifa, Madaraka Nyerere mwaka 1996, ambapo walifanikiwa kupata watoto watatu.

Leticia alikuwa mtoto wa Mzee Musobi Mageni. Julai 27 2015, Leticia alitangaza kuihama CHADEMA na kurejea Chama Cha Mapinduzi (CCM).


Mungu ailaze roho ua Marehemu mahali pema, Amina.
Previous Post Next Post