WEMA SEPETU ATHIBITISHA KUINGIA KWENYE KINYANG'ANYIRO CHA KUGOMBEA UBUNGE, HII HAPA KAULI YAKE

Wema Sepetu
Wema:“…. Yes nimefanya so ama nilikuwa nazungumza na mangement yangu ambayo yupo Martin kadinda na pia yuko Petiman ambaye yupo katika suala zima la kampeni yangu so watanzania wajue tu yes nitachukua fomu ya kugombea Ubunge wa viti maalumu ya mkoani Singida and tutaona uko mbele itakavyokuwa kwasababu hiki ni kinyang’anyiro naingia katika ni kama vile naingia kwenye mapambano yaani vitaani so kuna kupata na kukosa lakini si fikiri kukosa kwasababu mtu ukifikiri kukosa unajiweka kwenye negative side sana lakini najua kwa nguvu za watanzania na kwa nguvu za wananchi wa Singida wataweza kuniamini na kunipa kura zao".

Katika mahojiano hayo Wema Sepetu amezungumza kuhusu ishu ya kuwa na mahusiano na boyfriend wa Lina alisema "...Huwezi amini hizo habari si za kweli kwasababu tulikuwa tunafanya project zinakuja ila nimeshangashwa kuona kwanini Lina ameenda on air kwenye kipindi na kuzungumza hizo habari kuwa natembea na boyfriend wake naomba watu waelewe kwamba sikweli…”

Hivi sasa Wema Sepetu yupo mkoani Singida kwenye maandalizi ya kuchukua fomu ya kugombea Ubunge kupitia chama cha mapinduzi kupitia Viti Maalumu. Pia Wema amejiandikisha katika Daftari la wapigakura mkoani humo kwa kuwa ndio Mkoa atakao gombea na pia Mama mzazi ni mzawa wa mkoa huo. Hivi sasa kazi aifanyayo ni ya ushawishi kwa vijana wajitokeze katika kujiandikisha kwenye daftari hilo la kudumu la wapiga kura.
Previous Post Next Post