AMINA MWIDAU (VITI MAALUMU CUF) NDIYE MWENYEKITI MPYA WA KAMATI YA PAC

Amina Mwidau
Mwenyekiti mpya wa Kamati ya PAC, Amina Mwidau (Viti Maalumu Mkoa wa Tanga CUF).

MBUNGE wa viti maalum Mkoa wa Tanga, Amina Mwidau (CUF) ndiye Mwenyekiti mpya wa Kamati ya PAC baada ya aliyekuwa mwenyekiti wake, Zitto Kabwe kung'atuka kwenye nafasi yake ya ubunge.



Kupitia akaunti yake ya Facebook, aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema) na Mwenyekiti wa Kamati ya PAC ambaye jana alijiunga rasmi na Chama cha ACT-Tanzania, Zitto Kabwe amempongeza Amina kwa imani aliyopewa na wajumbe wenzake wa Pac.
"Nimefanya kazi na Amina tangu mwaka 2010 tulipokuwa kamati ya POAC na nina imani, kwa ushirikiano mkubwa wa Makamu Mwenyekiti ndugu Deo Filikunjombe wataendeleza kazi tuliyoianza ya kujenga mfumo madhubuti wa Uwajibikaji nchini kwetu" aliandika Zitto Kabwe.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post