Unknown Unknown Author
Title: WEZI WAKWAPUAJI WA SIMU KWA PIKIPIKI WANUSURIKA KUCHOMWA MOTO
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Ule usemi wa za mwizi ni arobani ,umetimia leo baada ya vijana wawili wanaotumia pikipiki (majina yao hayakupatikana mara moja) wenye uta...
ajali ya moto
Ule usemi wa za mwizi ni arobani,umetimia leo baada ya vijana wawili wanaotumia pikipiki (majina yao hayakupatikana mara moja) wenye utaalamu wa hali ya juu wa kukwapua simu za mikonini za watu wawapo kwenye magari au hata watembea kwa miguu kushindwa kufurukuta mbele ya wananchi wenye hasira.

Tukio hilo limetokea jioni hii mbele ya bustani ya Botanical kwa upande unaotazamana na geti kuu la kuingia Hospitali ya Ocean Road, baada ya kumkwapulia simu mwanadada mmoja (jina kapuni) aliekuwa akitembea kwa miguu na kwa bahati nzuri kulitokea msamalia aliekuwa na gari yake akaliona tukio zina na hapo ndipo alianza kuwafukuzia na mwisho wa mbio hizo ndio ukafika hapa baada ya kuzidiwa maarifa na pikipiki yao, hali iliyowapelekea kuanguka eneo hilo. Vijana hao walikamatwa na pikipiki yao ikachomwa moto.

ajali ya motoMmoja wa mashuhuda wa tukio hilo,akiwasimulia watu waliofika kwenye tukio hilo namna mambo yalivyokuwa mpaka kufikia kuchomwa moto kwa pikipiki hiyo yenye nambari za usajili T 636 CXX.
ajali ya motoTaswira za kuwaka moto kwa pikipiki hiyo zikiendelea kuchukuliwa.
ajali ya moto
Mdau akijipatia Selfie mbele ya pikipiki iliyokuwa ikiteketea kwa moto wakati huo.

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top