Kwa mujibu wa wa taarifa ya Uongozi wa TRL iliyotolewa Februari 16, 2015 uamuzi wa treni kutofika katika stesheni ya Kigoma unatokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha mjini Kigoma na hivyo kuzoa mchanga ambao umefunika tuta la reli katika eneo la stesheni ya Kigoma.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo abiria wote wanaowasili na wale wanaondoka Kigoma itawalazimu kujitegemea usafiri kwenda makwao na pia wale watakaosafiri kuja Tabora na Dar es Salaam kwa kutumia kituo kidogo cha Katosho.
Mara baada ya hali kutengemaa na kurekebishwa miundo mbinu ya reli katika stesheni ya Kigoma huduma zitarejeshwa kama kawaida.
Aidha Uongozi wa TRL unawaomba radhi wateja wake na wananchi kwa jumla hasa wa mkoa wa Kigoma kwa usUmbufu utakajiotekeza .
Imetolewa na Afisi ya Uhusiano ya TRL kwa Niaba ya
Mkurugenzi Mtendaji ,
Mhandisi Kipallo Aman Kisamfu
Dar es Salaam,
Februari 18, 2015
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.