‘Daktari:Jk muokoe Ray C’ ndio kichwa cha habari cha magazeti iliyomtoa macho Rehema Chalamila aka Ray C iliyoandikwa na gazeti liitwalo ‘Amani’ katika kurasa zake wa mbele.
kupitia kwenye ukurasa wake wa Instagram leo saa chache zilizopita amepost picha ya gazeti lenye stori hiyo na kuandika; "MLISEMA NITAKUFA BAADA YA SIKU 190 HAYA HATA BADO SIKU HAIJAFIKA MNAANDIKA TENA HUU UPUUZI, HIVI NYIE MNATAKA KUNIULIA MAMA YANGU JAMANI? HAYA SASA MAMA YANGU PRESHA JUU USO WOTE UMEMVIMBA SABABU YA PRESHA KISA HILI GAZETI LENU! MBONA HAMNIONEI HURUMA MWENZENU BADO. HATA SIJAMALIZA MATIBABU MNAANZA KUNIOMBEA MABAYA! KAMA MNATAKA KUNIUA NITAFUTENI MNICHOME HATA KISU NIFIE MBALI LAKINI SI MAMA YANGU!!, NAANDIKA HII MESEJI CHOZI LINANITOKA! NAWAOMBA MSINIULIE MAMA YANGU KWAPRESHA NA HIZI HABARI ZENU……
MSINIOMBEE MABAYA MWENZENU NIMEPITIA KWENYE MTIHANI MGUMU SANA KWENYE MAISHA YANGU, KAMWE SITORUDI NYUMA, NAOMBA SAPOTI YENU….MSINIOMBEE MABAYA’ —- @rayc1982
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.