Unknown Unknown Author
Title: CROUCH AKATAA KUREJEA LONDON KUJIUNGA NA BOSI WAKE
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Mshambuliaji kutoka nchini England, Peter James Crouch amezima ndoto za aliyekua meneja wake Tony Pulis za kutaka kumuhamisha huko Stoke O...
Mshambuliaji kutoka nchini England, Peter James Crouch amezima ndoto za aliyekua meneja wake Tony Pulis za kutaka kumuhamisha huko Stoke On Trent na kumpeleka jijini London kwa ajili ya kujiunga na klabu ya Crystal Palace.
Peter James Crouch
Crouch, amezima ndoto hizo baada ya kukubali kusaini mkataba mpya wa kuendelea kuitumikia klabu ya Stoke City ambao utamuweka klabuni hapo mpaka mwaka 2017.

Pulis, alitarajia kumsajili mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 33 kama mchezaji huru mwishoni mwa msimu huu, kufuatia mkataba wake wa awali kutarajia kufikia kikomo mwishoni mwa msimu huu.

Hata hivyo Crouch aliungana na mchezaji mwingine wa Stoke City, Glenn Whelan ambaye amakubali kuongeza mkataba mpya kwa muda wa miaka miwili ijayo.

Tonny Pulis wakati akiwa meneja wa Stoke City alimsajili Crouch mwaka 2011 akitokea kwenye klabu ya Tottenham Hostpurs ya jijini London.

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top