Zuriel Oduwole, umri wake ni miaka 12, ameweka historia nyingine baada ya documentary yake ya ‘A Promising Africa’ kuwa documentary ya binti mdogo zaidi duniani kuonyeshwa katika majumba makubwa ya cinema.
Jarida la Forbes lilimtaja kuwa msichana mdogo mwenye asili ya Afrika ambaye ni miongoni mwa watu 100 mashuhuri wenye ushawishi zaidi Afrika waliotajwa kwa mwaka 2013 wakiwemo Marais watatu, pia akawa na rekodi ya kuwa mtu mdogo zaidi dunia kuandikwa historia yake katika Jarida la Forbes.
Documentary hiyo itaonyeshwa London, Januari mwaka huu na baadaye itaanza kuuzwa.
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.