Unknown Unknown Author
Title: HII HAPA ORODHA YA RAPPERS 10 WALIOWAHI KUWASALITI WAKE/WAPENZI WAO
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Wiz Khalifa hajawa Rapper wa kwanza kumsaliti mpenzi wake.Inasemekana hii ni kawaida kwa rapper kukamatwa wakisaliti wake na wapenzi wao. ...
Wiz Khalifa hajawa Rapper wa kwanza kumsaliti mpenzi wake.Inasemekana hii ni kawaida kwa rapper kukamatwa wakisaliti wake na wapenzi wao. Hii list ya wasanii kumi wa Rap waliowahi kuhusishwa na usaliti.
Wiz Khalifa

Rapper Wiz Khalifa ameachana na Amber Rose baada ya Wiz kufumaniwa akiwa na mwanamke kitandani. Wanawake hao ni mapacha.
Swizz Beats
Kabla ya Swizz Beatz kuwa na Alicia Keys,aliwahi kutoka na msanii wa rnb Mashonda, Kwenye barua ndefu aliyoandika Mashonda miaka mitano iliyopita alisema Alicia Keys ndio aliyevunja ndoa yake na Swiz Beats.
Ja Rule
Ja Rule alimsaliti Karrine ‘Superhead’ kwenye kitabu alichoandika dada huyu anasema Ja Rule alimsaliti mpaka ilifikia hatua akazoea tu. Kiabu kinaitwa Confessions Of A Video Vixen.
P.Didy
Kim Porter amekuwa akitengana na kurudiana na rapper/mfanya biashara Diddy alisema mwaka 2007 kwenye interview na Essence kuwa usaliti wa Puff daddy na wanawake kama Sarah Chapman na kumpa ujauzito ndio sababu ya kuvunjika kwa mahusiano yao.
B.I.G
Biggie na Faith Evans walifunga ndoa mwaka 1994 na baada ya furaha ya muda mfupi, Biggie alianzisha mahusiano na msanii wake Lil Kim.
Big Boi
Big Boi alimsaliti mke wake Sherlita M. Patton wa miaka 11 kwenye ndoa.
Criss Brown
Chris Brown ni miongoni mwa wasanii wa rnb waliomsaliti Rihanna kwa muda mrefu huku dunia ikijua kuwa mapenzi yao yana nguvu. Imefahamika kuwa Chris alikuwa na Karrueche wakati yupo na Rihanna pia.
Ja Rule
Nas na Kelis walipeana talaka 2010. Sababu ya talaka yao ilikuwa usaliti wa Nas ambao aliwahi kuhojiwa na kutubu kuwa uaminifu na usaliti ndio umevunja ndoa yake.
Faborous
Kwa kuwa ilikuwa siri kwa rapper Fabolous ila familia ya mama wa mtoto wake Emily B iliweka wazi kuwa mtoto wao alisalitiwa sana na rapper huyu mpaka kupelekea kutengana.
Fat Joe
Mwaka 2012 Mke wa Fat Joe alitaka talaka yake baada ya kuka kwenye ndoa kwa miaka 17. Hii ni baada ya Fat Joe kuhusika kimapenzi na Ms. Dubai.


********************************************
LindiYetu.com ndio mtandao wako kwa habari za burudani, Siasa, Michezo ya Africa na Nje, Tuwe pamoja huku pia >> Instagram Twitter Na Facebook

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top