Rooney, ametoa msisitizo huo kupitia ukurasa wake katika mtandao wa kijamii wa Facebook, ambapo ameandika ana mtazamo tofauti na jinsi ambavyo watu wanavyo wachukulia Man Utd, kutokana na matokeo mabaya ya mwishoni mwa juma lililopita baada ya kufungwa na klabu ya Leicester City mabao 5-3.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 28, ameongeza kuwa kila anapowangalia wachezaji waliopo kwenye chumba cha kubadilishia nguo, anaona vipaji ambavyo vikichanganywa na umakini wa meneja wao hana shaka kwamba klabu hiyo itapata mafanikio.Man Utd, imekuwa haifanyi vizuri tangu mwanzoni mwa msimu huu na mpaka sasa imeshapoteza michezo miwili, kutoka sare mara mbili na kushinda mmoja
HII NDIO POST YENYEWE::
Cjawapata fresh anamasha kwamba man aiwez kupanda ksa wachezaj uwezo mdogo au hana mashaka anaona inawachezaj wazur na itafanya vyema tu
ReplyDelete