
Basi la Kampuni ya AHIDA"S
lenye namba za usajili T 231 BHC linalofanya safari zake za kila siku Kutoka Dar - Lindi - Tunduru Limepata ajali mapema asubuhi ya leo katika eneo la kijiji cha Kinyanya - Kibiti na Kusababisha Vifo zaidi ya 3 na majeruhi. Ajali hiyo ilitokea baada ya Dereva wa basi hilo kumkwepa mtoto aliyekuwa anakatiza barabara.
Mara baada ya kutokea ajali hiyo dereva aliweza kujisalimisha kituo cha polisi cha Kibiti. Basililikuwa likitokea Dar es salaam kwenda Tunduru.


Tags
HABARI ZA KITAIFA